Wednesday, January 24, 2018

Published January 24, 2018 by with 0 comment

Halima Mdee amtaka Jaji Mkuu kuingilia kesi ya Sugu

Mbunge wa jimbo la Kawe (CHADEMA) Halima Mdee amefunguka na kumuomba Jaji Mkuu Prof. Ibrahim Hamis Juma kufuatilia mwenendo wa kesi za kisiasa nchini na kudai kuwa baadhi ya mahakimu wamekuwa wakipindisha mambo kwa sababu za kisiasa.

Halima Mdee amesema hayo wakati akiongea na kituo cha EATV na kusema kuwa Jaji Mkuu anaposema wanasiasa wasiingilie Mahakama hivyo na yeye anapaswa kusimama na kuhakikisha kuwa Mahakimu wakitenda haki na kukemea wale ambao kwa makusudi wamekuwa wakipindisha haki za watu.

"Ni zaidi ya wiki sasa Mhe. Sugu yupo ndani lakini amenyimwa dhamana kwa kosa ambalo linadhaminika kisheria na kiutaratibu kwa mujibu wa sheria zetu kama kosa linadhaminika ni wajibu wa polisi kutoa dhamana na polisi wakikushikilia ndani ya zile saa 48 wakikupeleka mahakamani ni jukumu la Mahakama kufanya hivyo sasa suala la Sugu limeenda Mahakamani ambapo huo ndiyo muhimili pekee ambao tunautegemea .

"Sasa unapokwenda Mahakamani sehemu pekee ambayo unaitegemea kupata haki halafu unaona hiyo haki haipatikani kwa makusudi kabisa hivyo Jaji Mkuu na yeye anapaswa kuyatambua haya na kuwakemea baadhi ya Mahakimu ambao wanafanya vitu kama hivi" alisema Mdee

Mbali na hilo Halima Mdee amedai kuwa kuna tetesi za kutaka kumfunga Mbunge wa Mbeya Mjini Mhe. Joseph Mbilinyi “Sugu' kama ambavyo alifungwa Mbunge wa Kilombero, Peter Lijualikali.
Read More
      edit
Published January 24, 2018 by with 0 comment

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya January 25

Read More
      edit
Published January 24, 2018 by with 0 comment

Shahidi aeleza alivyomrekodi Sugu

Mvutano wa kisheria katika kesi inayowakabili mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ na katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga umeibuka kwa mawakili wa pande mbili kuhusiana na ushahidi wa sauti iliyorekodiwa kwa kinasa sauti ambao upande wa Jamhuri uliiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi-Mbeya kuusikiliza na upande wa utetezi kuupinga.

Mvutano huo umeibuka baada ya shahidi wa tano upande wa Jamhuri, Inspekta Joram Magova akiongozwa na wakili wa Serikali mkuu, Joseph Pande kudai kwamba ndiye aliyefanya kazi ya kurekodi sauti za Sugu na Masonga kwenye mkutano wao wa Desemba 30 mwaka jana hivyo kuiomba Mahakama kupokea kifaa kilichotumika kurekodia kama kielelezo cha pili kilichowasilishwa na shahidi wa wanne, askari Daniel Masanja katika ushahidi unaondelea kutolewa mahakamani hapo.

Upande wa utetezi ukiongozwa na mawakili Boniface Mwabukusi na Hekima Mwasipu waliupinga ushahidi huo wakiiomba Mahakama kutoupokea wala kusikiliza wakidai shahidi aliyetoa kifaa hicho ana masilahi na kesi hiyo hivyo wanaona ushahidi huo haujakidhi matakwa kisheria.

Hata hivyo, mawakili wa Serikali, Pande na Baraka Mgaya kwa nyakati tofauti, waliinuka na kupinga hoja zilizotolewa na mawakili wa utetezi kwa hoja kwamba walichoiomba mahakama hiyo ni kusikiliza maudhui yaliyomo kwenye kifaa hicho ambacho kimewasilishwa kama kielelezo na kimepokewa.

“Shahidi anapaswa kuwa yule aliyeona, kushuhudia na aliyefanya na kusikia. Sasa hawa wenzetu wanataka kutuaminisha kwamba shahidi siyo yule aliyeona, aliyesikia na kufanya na kushuhudia, kitu ambacho sicho. Kama kielelezo kimepokewa na Mahakama hivyo hoja kwamba kisisikilizwe kilichomo ndani yake, itakuwa imepokea ya nini wakati hatujui kilichomo? Hivyo mheshimiwa hakimu naomba hoja hii itupiliwe mbali.”

Kifaa hicho kilitolewa na shahidi wa wanne Masanja ambaye alidai ndiye aliyekipokea na kukihifadhi katika chumba cha kuhifadhia vielelezo vyote vinavyotakiwa kutolewa ushahidi mahakamani katika Ofisi ya Upelelezi Mkoa wa Mbeya (RCO).

Shahidi huyo aliongozwa na wakili wa Mgaya na mahojiano yalikuwa:

Wakili: Shahidi hebu tueleze wewe ni nani na unafanya kazi ofisi gani.

Shahidi: Ni askari polisi nafanyia Ofisi ya Upelelezi Mkoa wa Mbeya (RCO) lakini vilevile ni mtunza vielelezo katika ofisi hiyo.

Wakili: Tangu lini unafanya kazi hiyo?

Shahidi: Tangu mwaka 2004.

Wakili: Vielelezo gani unavyotunza?

Shahidi: Vielelezo vya kesi inayopelelezwa na kuna aina mbili, kwanza vielelezo ambavyo vimeshafunguliwa kesi na pili vielelezo ambavyo kesi yake inakuwa haijafunguliwa mahakamani.

Wakili: Ieleze Mahakama Desemba 30 mwaka jana ulikuwa wapi na ulikuwa unafanya nini?

Shahidi: Siku hiyo majira ya saa 12 jioni nilikuwa nyumbani lakini nikapigiwa simu na Inspekta Joram akinihitaji ofisini niweze kupokea vielelezo.

Wakili: Ulifanyeje baada ya hapo?

Shahidi: Ilinibidi niende na baada ya kufika ofisini nilimkuta Inspekta Joram akanieleza kuna vielelezo vya kuhifadhi, ametoka kwenye mkutano.

Wakili: Mkutano gani?

Shahidi: Mkutano wa Chadema.

Wakili: Ulifanyika wapi?

Shahidi: Ulifanyika maeneo ya Ruanda Nzovwe.

Wakili: Kielelezo gani ulichopokea?

Shahidi: Ni tape recorder.

Wakili: Baada ya kukueleza hivyo ulifanya nini?

Shahidi: Baada ya kuelezwa hivyo, nikavihifadhi kwa kuvifungia kwenye kasiki ofisini.

Wakili: Hebu ieleze Mahakama, Januari 2 mwaka huu ulikuwa wapi na kufanya nini?

Shahidi: Nilikuwa ofisini kwangu nikiendelea na majukumu yangu na akaja Inspekta Joram akihitaji tape recorder ile kwa ajili ya kwenda kuwasikilizishia viongozi wa Chadema akiwamo mbunge (Sugu).

Wakili: Baada ya hapo nini kiliendelea?

Shahidi: Inspekta Joram aliendelea na mahojiano na viongozi hao hadi saa nane mchana akanirudishia kifaa hicho nami nikakihifadhi kwenye kasiki.

Wakili: Tokea siku hiyo ulipokabidhiwa hadi leo (jana) hii nini kiliendelea?

Shahidi: Niliendelea kuhifadhi hadi leo (jana) nilioambiwa vinahitajika mahakamani.

Wakili: Ukiviona unaweza kuvitambua?

Shahidi: Ndiyo.

Wakili: Unahitaji Mahakama ifanyie nini vielelezo hivi?

Shahidi: Naomba Mahakama ivipokee kama vielelezo vya ushahidi katika kesi hii.

Wakili: Mheshimiwa Hakimu, shahidi wetu anaomba vidhibiti hivi vyote vipokewe na Mahakama yako kama vielelezo katika kesi hii.

Baada ya wakili kumuongoza shahidi huyo, Wakili Mwabukusi wa utetezi alisimama na kuweka pingamizi juu ya kielelezo hicho akipinga kisipokewe kwa madai kwamba hakijakidhi matakwa ya kisheria na hakina ubora unaotakiwa.

“Kifaa kinachotaka kuwa kielelezo mahakamani hapa ni kifaa ambacho kinasemekana kina maelezo yaliyorekodiwa na mtu mwingine na huyu aliyerekodi hatujaambiwa alirekodi kwa maudhui gani,” Mahakama haijaelezwa kwa namna gani ‘data massage’ zilizomo katika kifaa hiki hazijawa ‘tempered’ na haziwezi kuwa ‘tempered’ kwa namna gani. Tunapinga kifaa hiki kisipokewe kwa vile hakijakidhi matakwa na hakina ubora unaotakiwa kisheria.

Baada ya hoja hizo za Wakili Mwabukusi, Wakili wa Jamhuri, Pande aliinuka na kusema msingi wa hoja hizo unapinga kutolewa kwa kifaa hicho kama ushahidi kwa madai kwamba shahidi aliyewasilisha si aliyerekodi kwamba hawana pingamizi ikiwa kitatolewa na shahidi anayefuata ambaye kimsingi atakitambua.

Hata hivyo, mawakili wa utetezi walipinga hoja za wakili huyo na kutaka visipokewe vyote

Mabishano hayo yalidumu kwa takriban nusu saa kabla ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Michael Mteite kuahirisha kesi hiyo kwa nusu saa ndipo atoe uamuzi juu ya kinachobishaniwa.

Baada ya kurejea, Hakimu Mteite alisema Mahakama imejiridhisha kwamba vielelezo hivyo vinaonekana katika muonekano wake halisi, hivyo inavipokea kama vidhibiti na itatoa ufafanuzi wa kwa nini iliamua kuvipokea siku ya hukumu ya kesi yenyewe. Kesi hiyo inaendelea leo.
Read More
      edit
Published January 24, 2018 by with 0 comment

Kamati ya Bunge yatoa agizo mifuko ya plastiki Ipigwe Marufuku

Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira imeiagiza Serikali kupiga marufuku matumizi ya mifuko ya plastiki kutoka nje ya nchi ili kulinusuru Taifa na madhara yanayotokana na mifuko hiyo.

Maagizo hayo yalitolewa baada ya kamati hiyo jana kukutana na Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji.

Akizungumza jana, mwenyekiti wa kamati hiyo, Sadiq Murad alisema walipata maelezo kutoka serikalini kuwa uzalishaji katika viwanda 41 vya plastiki nchini ulikuwa ni tani 73 katika mwaka 2016.

Hata hivyo, alisema mifuko iliyoingia nchini kupitia bandarini na mipakani ilikuwa tani 1,375.

“Kamati ilishauri ipigwe marufuku mifuko ya plastiki kutoka nje ya nchi na iwekwe tahadhari katika mipaka yetu,” alisema.

Alisema kamati inaitaka Serikali kufanya uhakiki wa uzalishaji katika viwanda vya nchini ambavyo vimepunguza uzalishaji ili waweze kukaa chini na kuzalisha mifuko ambayo itakayokidhi mahitaji na vigezo.

“Na hii itakuwa ni ya muda kuzalisha mifuko hiyo kwa masharti ya vigezo baadaye Tanzania isiwe na uzalishaji wa mifuko hii tena inayoharibu mazingira,” alisema.

Murad alisema zipo nchi nyingine kama Kenya, Rwanda, Uganda na Zanzibar ambazo zimepiga marufuku uzalishaji na uingizaji wa mifuko hiyo na kutafuta mifuko mingine inayotengenezwa na nguo, karatasi na majani.

Alisema mfano mzuri ni Zanzibar ambayo imepiga marufuku mifuko hiyo tangu mwaka 2016 na mtu anapoingia na mifuko hiyo bandarini hunyang’anywa na kupewa mingine.

“Tueleweke kabisa sisi kama kamati hatutaki kiwanda chochote kifungwe, tunataka uzalishaji kwa kufuata masharti na vigezo. Tunaunga mkono juhudi za Rais John Magufuli za kuipeleka nchi katika uchumi wa viwanda lakini vigezo na masharti lazima yazingatiwe,” alisema.

Akizungumzia agizo hilo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba alisema hawaja japelekewa rasmi hayo mapendekezo. Hata hivyo alisema watapiga marufuku mifuko yote ya ndani na nje. “Wenye viwanda wajiandae maana yake dhamira ya Serikali wanaijua tangu mwaka 2016,” alisema
Read More
      edit
Published January 24, 2018 by with 0 comment

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya January 24

Read More
      edit

Monday, January 22, 2018

Published January 22, 2018 by with 0 comment

Serikali Yamkana Nabii Tito, Viongozi Dini Wataka Achukuliwe Hatua

Mkurugenzi wa Idara ya Huduma za Sheria wa Wizara ya Mambo ya Ndani, Marlin Komba amesema hamtambui  mtu anayejiita nabii Tito na kwamba hajasajili kanisa lake katika ofisi ya msajili wa taasisi za dini.

Komba amesema Serikali imeona vitendo anavyovifanya ‘nabii’ huyo kupitia mitandao ya kijamii na imeanza kuchukua hatua.

“Ninachoweza kusema ni kwamba hakuna mtu anayezuiwa kuongea hapa nchini, mwache aongee anavyoweza ila Serikali imeshaona anachokifanya na yanayoendelea mitandaoni  hatua zinachukuliwa dhidi yake,” amesema Komba.

Kwa upande wao viongozi wa dini wameonyeshwa kukerwa na kulaani vitendo anavyovifanya mtu huyo anayejiita nabii na kusisitiza kuwa hakuna dini inayoruhusu hayo.

Msaidizi wa Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT) Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Mchungaji Chediel Lwiza amesema kwa vitendo anavyofanya mtu huyo hapaswi kujiita mtumishi wa Mungu.

“Huyo hawezi kuwa mtumishi wa Mungu na wala hafanyi huduma ya kanisa ni vyema watu kama hawa wafuatiliwe na hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao. Natumaini Wizara ya Mambo ya Ndani ambayo ndani yake ina ofisi ya msajili wa taasisi za dini itafanya kazi yake.”

Lwiza ametumia fursa hiyo kuwasisitiza Watanzania kwenda kwenye makanisa ya kweli yanayozingatia neno la Mungu.

Amesema, “Hakuna sababu ya kutangatanga, Watanzania mkasali kwenye makanisa yanayotambulika na yanayosimamia na kufundisha neno la Mungu. Kuhangaika ndiko kunakowafanya wengine waangukie kwa watu kama hao. Wapo wanaojaribu kupotosha neno la Mungu lakini ukweli ni kwamba neno la Mungu halipotoshwi.”
Read More
      edit
Published January 22, 2018 by with 0 comment

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne ya January 23


Read More
      edit