Wednesday, September 21, 2016

Published September 21, 2016 by with 0 comment

Basi la Super Shem Lapata Ajali na Kuua watu 11 Jijini Mwanza Leo


Basi la Super Shem linalofanya safari za Mwanza kwenda  Mbeya limepata ajari ya kugongana na hiace katika kijiji cha Hungumalwa Mwanza na kusababisha vifo vya watu  wanaodaiwa kufika 11 asubuhi hii.


Kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo, wanaeleza kuwa Basi hilo liliigonga gari hiyo ndogo ambayo iliingia kwenye barabara kubwa bila ya kuwa na tahadhali, Juhudi za kumpata Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza zinaendelea kufanyika ili kuthibitisha tukio hilo.
Read More
      edit
Published September 21, 2016 by with 0 comment

Uamuzi wa CCM kuhusu Mwenyekiti wa UVCCM anayetuhumiwa kughushi nyaraka za Usalama wa Taifa

Read More
      edit
Published September 21, 2016 by with 0 comment

Mahakama ya Kisutu yamtaka Mhe.Tundu Lissu kufika mahakamani kujieleza kwa nini asifutiwe dhamana.


Mahakama ya hakimu mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam imemtaka mbunge wa Singida Mashariki kupitia CHADEMA, Mhe.Tundu Lissu anayekabiliwa na kesi ya uchochezi pamoja na wahariri wa gazeti la Mawio kufika mahakamani kujieleza kwa nini asifutiwe dhamana.

Hakimu Simba ametoa agizo hilo jana baada ya Lissu pamoja na mdhamini wake kutokuwepo mahakamani hapo kama sheria inavyotaka na hatua hiyo ilifikiwa baada ya wakili wa serikali kuomba itolewe hati ya kumkamata lakini hakimu Simba akamtaka Lissu aende kujieleza kwanini asifutiwe dhamana.

Katika kesi hiyo ya uchochezi, hakimu Simba alitoa uamuzi ambao umeuruhusu upande wa mashtaka kuyaleta upya mashtaka yanayofanana na yale yaliyoondolewa awali mahakamani hapo kutokana na kutokuwa na kibali cha mkurugenzi wa mashtaka (DPP) kwa kuwa ya sasa yanakibali na kuyatupilia mbali maombi ya Kibatala.

Hakimu Simba alisema upande wa mashtaka walikuwa na haki ya kurekebisha mapungufu na kuyaleta tena mashtaka hayo mahakamani.

Baada ya uamuzi huo kutolewa wakili Peter Kibatala alidai kuwa hawajaridhika na uamuzi huo watakata rufaa kuupinga kwa sababu wanaamini mashtaka hayo yalivyofutwa ilikuwa na maana ya kuwa yamekufa na akaiomba mahakama kutoyasoma mashtaka hayo mapya hadi rufaa yao itakaposikilizwa na mahakama kuu na kutolewa uamuzi.

Wakili wa serikali mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekwisha kamilika.

Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Mhariri wa gazeti hilo, Simon Mkina, Jabir Idrisa na mchapishaji wa kampuni ya Jamana, Ismail Mehboob ambao awali walikuwa wakikabiliwa na mashtaka matano likiwamo la kuandika habari za uchochezi kinyume na sheria ya magazeti ya mwaka 2002.

Chanzo: ITV
Read More
      edit
Published September 21, 2016 by with 0 comment

CUF kugharamia matibabu ya Maalim Seif

Wanachama wa Chama cha Wananchi (CUF)  wamesema wapo tayari kugharamia matibabu ya Katibu Mkuu wa chama chao, Maalim Seif Sharif Hamad.

Tamko hilo limetolewa siku chache baada ya kuibuka taarifa kuwa  kiongozi huyo amesusa gharama za matibabu zinazotolewa na Serikali ingawa ni haki yake kwa mujibu wa sheria kama kiongozi mstaafu.

Akizungumza   kwa niaba ya wanachama wenzake kisiwani Unguja jana, mmoja wa wanachama wa CUF, Ali Abdallah Issa, alisema wanashangazwa na baadhi ya watu kumpiga na kumsema kiongozi huyo ambaye alidai ni kiungo muhimu katika kuwaunganisha Wazanzibari.

“Maaalim ana haki zote za kuhudumiwa na Serikali na si vinginevyo. Lakini kwa manyanyaso na kusimangwa  kila kukicha sisi wanachama wa CUF tupo tayari kugharamia matibabu ya kiongozi wetu.

“Na hili si jambo geni, Maalim alikamatwa na kuwekwa kuzuizini.  Je, alipotoka  alikuwa akitibiwa na SMZ? Jibu ni hapana ni fedha zake mwenyewe binafsi pamoja na wana CUF ambao walikuwa mstari wa mbele kumhudumia kiongozi wetu nasi sasa tutafaya hivyo ikiwa SMZ imeshindwa,” alisema Ali.

Alisema kitendo cha Maalim Seif kusafiri nje ya nchi kwa matibabu bila ya huduma za Serikali hakileti picha nzuri.

Kuna hatari visiwa vya Zanzibar vikaingia katika mgogoro na kujengeka   chuki hasa kati ya CUF na CCM, alisema.

‘’Iwapo Maalim Seif amekwenda kwenye matibabu kwa gharama zake binafsi basi inasikitisha sana kuona ni jinsi gani Katiba inavyoanza kukiukwa na kwa kweli si jambo jema na halifai,” alisema.

Naye Is-hak Said Makame, alisema   Zanzibar imepita katika wakati mgumu hasa baada ya kutokea   migogoro ya siasa iliyotokana na Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba mwaka jana  na ule wa marudio uliofanyika Machi 20, mwaka huu.

“Maalim hawezi kusemwa na hata kuonekana ni kiongozi anayetibiwa kwa fadhila kama alivyotaka Rais Magufuli alipokuja hapa Unguja kwenye mikutano yake. Sasa tunasema sisi CUF tutamlinda kiongozi wetu kwa hali na mali,”alisema Makame.

Alipotafutwa  Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Uhusiano wa Umma wa CUF, Salim Biman  kujua  Maalim Seif  amepata wapi fedha kwa ajili ya safari ya nje ya nchi kutibiwa.

Alisema  hajui ni wapi kiongozi huyo alipopata fedha za matibabu.

“Katibu Mkuu amekwenda India kwa ajili ya uchunguzi wa kawaida wa afya yake lakini nasi hatujui ni wapi amepata fedha. Ila atakaporejea nchini itatolewa taarifa kwa kina kuhusu suala hili,” alisema Biman.

Maalim Seif yuko   India na anatarajiwa kujerea nchini siku chache zijazo.
Read More
      edit
Published September 21, 2016 by with 0 comment

Rais Magufuli atengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Udhamini ya Mfuko wa Pensheni wa LAPFi na kuvunja Bodi yote

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 21 Septemba, 2016 ametengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Udhamini ya Mfuko wa Pensheni wa LAPF Prof. Hasa Mlawa kuanzia leo.

Pamoja na kutengua uteuzi wa Prof. Hasa Mlawa, Rais Magufuli amevunja Bodi ya Udhamini ya Mfuko huo.

Uteuzi wa Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Udhamini ya LAPF utafanywa baadaye.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

21 Septemba, 2016
Read More
      edit
Published September 21, 2016 by with 0 comment

Aliyemuua Trafiki Afikishwa Mahakamani


Mkazi wa Mbezi Africana Dar es Salaam, Amani Elikana (32), amefikishwa   katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni akituhumiwa kumuua Askari wa Usalama Barabarani, Sajenti Mensali wa Kituo cha Polisi Mabatini – Kijitonyama.

Akisoma hati ya mashtaka jana mbele ya Hakimu, Caroline Kiliwa, Wakili wa Serikali, Amani Mghamba alidai  mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo Julai 22 mwaka huu eneo la Kijitonyama.

“Mtuhumiwa inadaiwa kwamba siku hiyo kwa makusudi  ulimuua askari mwenye namba D. 8254 Sajenti Mensali kinyume cha sheria ya Jamhuri ya Muungano,” alidai Mghamba.

Hakimu Kiliwa alisema mtuhumiwa hapaswi kujibu kitu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza kesi hiyo hivyo shtaka hilo liliahirishwa  hadi Oktoba 4 mwaka huu litakapotajwa tena.
Read More
      edit
Published September 21, 2016 by with 0 comment

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano ya Septemba 21

Read More
      edit

Tuesday, September 20, 2016

Published September 20, 2016 by with 0 comment

RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 9 & 10


MUANDISHI:EDDAZARIA 

Ilipoishia...
Dokta Williama aliendelea kuwasikiliza wakuu hawa wa polisi ambao vyeo vyao vinawatambulisha kama ma RPC kwenye mikoa yao.Lifti ikafunguka na wote wakatoka ndani ya lifti.Askari hao wakaendelea kwa mwendo wa kasi na kuingia kwenye ukumbi wa mikutano.Dokta William akajiweka sawa nguo zake na kuingia ndani ya ukumbi huu.Gafla macho yake yakatazamana na midomo ya bastola alizo elekezewa na wakuu wa polisi waliokaa kwenye viti vyao huku wakioneka kukasirishwa sana na uwepo wake

ENDELEA....
IGP bwana Gudluck Nyangoi akwaamuru wezake kuziweka silaha zao chini na wakati
“Karibu dokra Willian”
Bwana G.Nyangoi alizungumza huku akitabasamu na kumfanya dokta William kushusha pumzi nyingi,kidogo wasiwasi ukaanza kumpungua.

“Jamani huyu ni miongoni mwa wanajeshi wa umoja wa matiafa,yupo hapa nchini kwa ajili ya mafunzo wa madaktari wa jeshi letu juu ya jinsi gani wanaweza kumtengeneza sura bandia”

“Dokta,kwanza samahani kwa kukuvunjia ratiba zako kwa maana haikuwa katika ratiba zako leo kama nitakuitaji hapa”
“Bila samahani mkuu”
“Karibu ukae”

Dokta William akaka kwenye kiti alicho onyeshwa na bwana Nyangoi,akawaytizama makamanda wote waliopo ndani ya ofisi na hapakuwa na hata mmoja anaye mfahamu zaidi ya IGP Gudluck Nyangoi.

“Jamani kama munavyo jua,sisi kama jeshi la polisi tumekubwa na msiba mkubwa sana wakupoteza vijana wetu katika tukio la jana usiku,Pia ni aibu kubwa kwetu sisi kama jeshi la polisi kwa kushindwa kupambana na majambazi ambao,sijajua ni vipi tulishindwa kuwazuia na kusababisha maafa makubwa kama haya”

Ukimya ukatawala,huku akili ya Dokta William ikiwa inajaribu kupanga kitu cha kuzungumza kabla hajaulizwa kwani ametambua umuhimu wake wa yeye kuwa hapa ni kuwashauri viongozi waliopo humu ndani 

“Jamani ninawasililiza,nasubiri maoni yenu.Nini tufanye ili kuwakamata hawa watu na ninavyo sikia wao ni wasichana sasa sijajua inakuwaje wasichana kama hawa wanatushinda kirahisi rahisi?”

“Mkuu mimi ninaona,kwanza tudhibiti mipaka yote ya nchi jirani kwa maana kumbukeni kulikuwa na tishio la kundi la Al-Shabab kuivamia mlimani city.Sasa isije ikwa ndio hao wameanza kutekeleza mipango yao”

“Asante bwana Shaban Mbago,mwengine?”
“Mkuu mimi kuna swala ambalo bado silipatii picha,haiwezekani mpango ule wa kumsafirisha yele binti katika njia ya ardhini ulibumburuka.Swali ni je,ni nani aliye toa siri ile?”

Mapigo ya moyo ya dokta William yakaanza kwenda kasi,ila hakutaka kuiruhusu hali hii kuendelea kuundama moyo wake,akawatazama wakuu wa polisi waliopo eneo hili na kuwaona wengi wapo kimya kila mmoja akikosa cha kuzungumza.Dokta William akanyoosha kidole na bwana G.Nyangoi akampa ruhusa ya kuzungumza
“Wakuu wangu mimi ninajambo moja ninaomba nizungumze”
“Zungumza tuu,kwani ushauri wako ni mkubwa sana”

“Kuna hali ambayo inaendelea ndani ya jeshi lenu,kwa kipindi kifupi nilicho kaa katika nchi hii na kushirikiana na jeshi lenu nikagundua kuna hali amayo sio nzuri na endapo mukiacha ikikua na kukomaa,Siku hadi siku jeshi lenu litazidi kuzalilisha na kuteketea mwisho wa siku ile imani ya kusema kuwa Tanzania ni nchi ya amani itafutika katika vichwa vya watu wengi”

“Viongozi kwa viongozi hamuaminiani,hilo ni la kwanza.Pili viongozi mumekuwa ni watu wakuunda vikundi vikundi vya watu ambao munawatumia kwa maslai yenu binafsi na si ya taifa.Kwa mfano kuna magaidi ambao jeshi la polisi mulikuwa munawatafuta kwa kipindi kirefu sana.

Kutokana na uaminifu finyu wa baadhi ya viongozi magaidi wale wakaendelea kudumu na kuishi kwa kipindi kirefu pasipo serikali kuzungumza kitu cha aina yoyote.Kila mulipo kuwa munajaribu kwenda kuwakama walikuwa wanawakwepa na kubaki mukijiuliza mutafanya nini?”

“Kabla ya hichi kikao kuendelea,jiulizeni je hakuna wasaliti watako vujisha siri juu ya watu muna watafuta? Na kama wapo je kuna haja gani ya hichi kikao kuendelea kuwepo hapa?”

Ukumbi mzima ukakaa kimya,sura za makamanda wote wapolisi zikawa zikimtazama Dokta William ambaye amezungumza maneno ambayo wengi wao hawakuwa wanayafikiria kuyazungumza

“Musikalie kuunda tume kuchunguza vitu ambavyo munajua majibu yake kabla ya kuzungumza.Nyinyi ni jeshi,munatakiwa kuwa kitu kimoja na si kuwa katika mgawanyiko ambao utawakost garama ambazo si za msingi.Jaribuni kuiga baadhi ya mbinu za kijeshi katika mataifa makubwa yaliyo endelea,mfano Marekani na kadhalika.Nitatolea mfano mdogo tuu wa wa wale wanejeshi walio tumwa kwenda kumuua Osama Bin Laden,Gaidi ambaye sisi kama Israel alituumiza pia vichwa jinsi ya kumpata”

“Ila kikosi cha wanajeshi wachache walio tumwa kuumuua Osama,kilikuwa ni cha siri kubwa hata makamu wa raisi wa Marekani hakuwa analifahamu hilo,zidi ya raisi Obama na wasadizi wake,Na tukio zima lilipokuwa linaendelea walikaa kwenye chumba maalumu pasipo na mtu yoyote kuwa na mawasiliano ya simu ya mkononi,hata raisi mwenyewe alizuiwa kuwa na simu.

Huo ni mfano mdogo ila hapa hapa ninashanga muheshimiwa unaendeleza kikao ila kuna huyo bwana hapo anachati na simu chini ya meza,Je kuna umuhimu gani wa hichi kikao?”
Bwana Noel Muro akastuka na kuuingiza simu yake mfukoni baada ya kunyooshewa kidole na Dokta William.
“Muro ninaomba uzime simu yako”

Bwana G.Nyangoi alizungumza huku akimtazama bwana Muro
“Mkuu cha mwisho kukizungumza ninawaomba,muunde kikosi maaalumu cha siri kitakacho wa pambana na hili swala.Asanteni”
Dokta William akakaa kwenye kiti na viongozi wote wakampigia makofi wakimpongeza kwa ushauri wake alio utoa.

“Dokta Willim asante sana kwa ushauri wako mzuri sana.Mimi ningekuomba usaidiane na mimi kuunda kikosi kitakacho weza kuwasaka hawa majambazi.Nipo radhi kuwaishawishi serikali kuongezea mshahara”
Laiti IGP bwana G.Nyangoi angegundua mtu anaye muomba juu ya huo mpango ndio muhusika nambari moja wala asinge zungumza hayo maneno

                                             ***

Kutokana na uelewa mkubwa wa Agnes katika maswala ya usomaji wa ramani akaanza kuwaelekeza wezake jinsi ya kuingia katika benki kuu ya taifa BOT kufanya tukio wanalo taka kwenda kulifanya.Maelekezo yake hayakuwa magumu sana kwa wezake kuyaelewa,Kila mmoja alielewa vizuri na palipokuwa na swali wakawekana sawa
“Ag tumesha isoma ramani nzima je,jinsi ya kuingi hapo itakuwa vipi?” Anna aliuliza

“Hapa kikubwa cha kufanya ni kuvaa miili ya bandia”
“Kivipi tutavaa miili ya bandia?”
“Sio sote tutavaa miili ya bandi,ila kati yetu mmoja atavaa mwili ambao utamfanya aonekane kama bibi kizee,atakwenda ndani ya benki huku katika kifungo cha ngoo yake kuna kamera ndogo ambayo tutaifunga na jinsi anavyo kwenda sisi huku nyuma kupitia simu zetu tutaweza kuona jinsi madhari ya ndani na jinsi ulinzi ulivyo”
“Agnes naamini leo tutakuchosha na maswali mengi,je hiyo kamera itakuwaje kuwaje?” Rahab aliiuliza

“Ngoja nimsaidie kujibu,Kamera ambayo itatumika ni ndogo sana na ipo kama jicho fulani hivi ambako tunaweza kulibandika kwenye kifugo cha nguo pasipo mtu yoyote kujua”
Fetty alimjibu Rahab
“Kamera na mwili huo vitapatikana wapi?”
“Kuna muarabu mmoja pale kariakoo anauza hivi vitu  ila ni kwa siri sana,Japo duka lake linauza urembo wa vitu vya kupambia nyumba” Agnes alizungumza

“So ni nani atakwenda kununu?”
Wakaa kimya huku kila mmoja akiwa kimya.
“Mimi nitakwenda?” Halima alizungumza na kuwafanya wezake kumtazama
“Sawa,itabidi tukafanyie make up itakayo kubadilisha hata muonekano wako”  Anna alizungumza
“Mimi nitakufanyia make up” Rahabu alizungumza 

“Ok kazi inafanyika lini?” Agnes alizungumza
“Kazi ya kununu vitu inaanza leo”
“Je siku ya kwenda kupiga tukio ni lini?” Halima aliuliza
“Hata kesho ikiwezekana kikubwa ni kuwa makini na lile ambalo tunalifanya”
“Mmmm,tuacheni hali huko nje itulie”
“Tukiwaacha wakijipanga itatuwia vigumu.Kikubwa ni kupiga tukio litakao waliza miaka yote” Fetty alizungumza huku akiwatazama wezake

Wakaanza kazi ya kumfanyia ‘make up’ Halima,wakamvalisha wigi la nywele lilo mbadilisha muonekano wake na kuzidi kuwa mzuri zadi,wakamuweka nyusi bandia zilizo zidi kumpendezesha.Hadi wanamaliza Halima akawa tofauti sana na jinsi alivyo,akavalia suruali iliyo mbana makalio yake ya wastani na kuziachia hipsi zake kuonekana vizuri

“Haki ya nani,ningekuwa mwanaume Halima ningekutongoza”
Rahab alizungumza na kuwafanya wezake kucheka
“Kweli vile,cheki mtoto alivyo bomba.Unaweza kusema ameshushwa kutoka mbinguni kumbe kwa shabaha za bunduki ni mwengine kabisa”
“Hembu Rahab acha ujinga bwana”

“Sasa hivi ni saa tano asubuhi,tukikusindikiza hadi pale barabarani itatuchukua kama dakika ishirini si ndioa?” Fetty alizungumza
“Ndio”
“Oya shosti kama kuna uwezekano utujie na gari basi”
“Gari bila hela litatokea wapi,Mbinguni?”
“Ahaaa tuchangeni changeni hata kaVitz kamilioni tano” Rahab alizungumza
“Ok kila mmoja atoe Milioni moja”

Wakakubaliana kila mmoja akatoa milioni moja moja na kumkabidhi Anna,Safari ya kumsindikiza mwenzao ikaanza huku njia nzima wakiwa wanazungumza na kila mmoja akiwa na bastola yake kiunoni.Njia nzima wakawa na kazi yakusimuliana stori zisizo na kichwa wala migu,wakafanikiwa kufika barabarani na wao hawakutoka kabisa barabarani na kumuacha Anna asimame mwenyewe barabarani huku akiwa na pochi ndogo aliyo ining’iniza kwenye kwapa lake

Anna akaisimamisha gari ndogo,kwa bahati nzuri gari ikasimama,akapiga hatua za haraka hadi sehemu ilipo simama na kuzunguka upende wa dereva na kuwakuta vijana wawili
“Samahani kaka zangu?”
“Bila samahani mrembo?”
“Ninaombeni lifti mimi ninakwenda Dar es Salaam”
“Ingia twende kwani na sisi tunakwenda Dar”

Anna akaingia siti ya nyuma na gari ikaondoka,Rahab na wezake wakarudi kwenye handaki.Anna akamtumi wezake meseji
(JAMANI HAWA WAKAKA WANAVUTIA)
(Umeshaa anza,jua kilicho kupeleka achana na hizo habari) Halima akawa wa kwanza kuijibu meseji
“Sister unaitwa nani?” Jama mmoja aliye kaa pembeni ya dereva alizungumza

“Mimi ninaitwa,Hilda” Anna alidanganya
“Ahaa mimi ninaitwa Jackson na huyu kaka yangu anaitwa John”
“Nashukuru kuwafahamu”
“Wewe unafanya kazi gani?”
“Mimi ni mke wa mtuu,najaa nyumbani kwa mume wangu”
“Ahaa,daa kweli wewe ni mke wa mtu kwa maana unavutia sana”

“Asante”
“Sisi bwana ni waanya biashara wa madini,Tunatokea mererani”
“Ahaa hongereni”
“Sasa sijui leo tunaweza kuwa pamoja”
“Ahaa mume wangu bwana ana wivu sana”
“Ahaaa,kawaida mbona.Kila mmoja na chake”

Wakaendelea kuzungumza hadi wanafika maeneo ya Mbezi wakakuta msururu mrefu wa magari,Anna akastuka baada ya kuona askari wengi wakiwa wanakagua gari mmoja baada ya jengine.Askari wawili wafika wenye gari alipo Anna na kuwaomba wote watatu kushuka ndani ya gari jambo lililo anza kumuogopesha askari mmoja akawa amemkazi macho sana Anna akionekana kumtilia mashaka......

            SHE IS MY WIFE(NI MKE WANGU)……10

......Redio za upepo za polisi zikaanza kusikika zikiokoroma na sauti kali ikasikika
“Kunaajali ya moto huku kwenye magari ya mbele,Over”
“Tunakuja.Over”

Askari mmoja alijibu na kuwaacha Anna,John na Jackson wakirudi ndani ya gari.Wakisubiria foleni iweze kusogea.
“Hivi jamaa alisema kuwa kuna moto mbele” John aliuliza baada ya kuona watu wengi wakikimbilia mbele
“Hembu,ngoja”
Jackson akashuka ndani ya gari na kukimbilia mbele,akakuta gari moja ndogo aina ya Subaru ikiwaka moto na wananchi wakijitahidi kuzima gari hiyo.Jackson akarudi kwenye gari

“Kuna gari hapo mbele inateketea”
“Ipo kwenye foleni” Anna aliuliza
“Ndio Hilda”
“Hakuna aliye jeruhiwa”
“Sidhani kwa maana hakuna mtu yoyote ndani ya gari”
Hali ya foleni ikazidi kuongezaka na kusababisha msongamano mkubwa wa magari
“Napoteza muda tuu”

Anna alijiseme kimoyo moyo huku akitazama nyuma kuyaangalia mabasi mengi yanayo tokea mkoani yakiwa yemejipanga kwa wingi yakisubiria gari za mbele kusogea.
“Jamani ngoja nikanunue maji pale dukani”
“Lete pesa yako nikakununulie,maji” Jackson alizungumza
“Hapana wee acha tuu nitanunua tu hapo juu”

Anna akashuka kwenye gari na kuvuka upande wa pili wa barabara huku akiwa makini asiweze kugundulika kirahisi, kwa kuzuga akaingia kwenye duka moja na kuagiza maji makubwa ya chupa, akiwa anasubiria kukabidhiwa maji na muuzaji akastuka baada ya kuona picha ya Fetty ikitangazwa kwenye taarifa ya habari kwenye kituo cha ITV

(JAMBAZI HUYU, NA WENGINE BADO WANAENDELEA KUTAFUTWA NA JESHI LA POLISI.KIKOSI MAALUMU.UKIMUONA SEHEMU YOYOTE TUNAKUOMBA UWASILIANE NA JESHI LA POLISI KUPITIA NAMBA YA SIMU +225 657072588)

Muandishi wa habari alizungumza na kumfanya Anna kubaki akitazama chini, akakabidhiwa maji na kutoa noti ya shilingi elfu kumi na kuondoka kabla hajapia hatua hata tano akastukia akiitwa na sauti ya kiume nyuma
“Dada umesahau chenchi yako”

Jamaa mmoja, aliye simama kando ya duka alimuambia Anna ambaye anatumia jina la bandia la Hilda.Anna akarudi haraka haraka hadi dukani na kuichukua.Akawatazama Jackson na John ndani ya gari na kuwaona wamejilaza kwenye siti zao huku kila mmoja akiwa amejochokea kiasi kwamba anatamani gari lake liruke hadi mbele kusipo kuwa a foleni na kuendelea na safari zake.

Anna akaanza kutembea kuelekea mbele kulipo tokea janga la moto huku macho yake yakiwa makini sana na polisi wanao wazudia watu kuisogelea sehemu ambayo gari linaungua na kuwaacha askari wa zima moto kufanya kazi hiyo.Akafanikiwa kupita pembezoni mwa barabara hadi sehemu walipo waendesha pikipiki(bodaboda)

“Kaka hapa hadi kariakoo ni bei gani?”
“Ahaaaa dada hapo kwa kumi natano”(elfu kumi na tano)
“Powa twende”
Anna akapanda kwenye pikipiki
“Naomba Helmet”
Akapewa Helment na kulivaa, safari ikaanza huku kila mmoja akiwa kimya.
“Kaka usipeleke kasi sana,nyinyi waendesha pikipiki siwamini”

“Kwa nini hutuamini?”
“Ahaaa nyinyi bwana pikipiki munajifunza leo kesho muingia barabarani”
“Ahaaa,wanao pataa ajali ni wale wazembe, utakuta mtu anaendesha pikipiki huku akiwa amekunywa konyagi, sasa ni kwanini asipate ajali”

Anna akalitazama eneo la kituo cha gesi ambacho jana walifanya tukio, na kuwaona baadhi ya askari wakifanya fanya uchunguzi wa vitu vidogo vidogo
“Ahaaa jana hapa kulichimbika” Dereva pikipiki alizungumza
“Kulikuwa na nini?” Anna aliuliza kama vile hajui kilicho tokea
“Ahaa nasikia kuna majambazi walifunga mtaa jana, hapakuwa na askari aliyekurupuka”

“Ahaaaa......!!”
“Ina maana jana hukusikia?”
“Mimi ninatokea,turiani Morogoro na wala sijasikia”
“Ahaaa,jana basi askari wengi wamekufa pale kwa kulipukiwa na gesi”
“Kisa nini hadi wakafa?”
“Ahaaa nasikia kuna sister mmoja ambaye ni jambazi, askari walimshika.Kumbe yule dada ni mafia katika kupambana pambana nao basi akawatoka polisi na sijui alifanyaj fanyaje hadi akailipua mitungi ya gesi”
“Ahaaa masikini weee”
“Ahaaa wee acha tuu, hapo ndipo nimeamini kuwa Tz kuna watu m agaidi kama huko Lebanon”
“Ahaaa pole yao”

Anna akaendelea kuzungumza na muendesha pikipiki hadi wanafika Kariakoo, Anna akatoa noti tatu za elfu kumi na kumkabidhi muendesha pilipiki
“Kaa na chenchi kwani safari ni ndefu”
“Asante dada yangu,Mungu akubariki”
“Amen”
Anna akaingia kwenye duka analo hitaji kununu vifaa na kumuacha muendesha pikipiki akiondoka zake.

Dokta William baada ya kumaliza kikao na viongozi wa polisi, akawaomba wampe muda kuweza kufikiria juu ya ombi lao la kuunda kikosi kipya cha uchunguzi ambacho kitawatafuta majambazi walio sababisha tukio la askari na wananchi kufariki.Kwa bahati nzuri likizo ya Dokta William inaanza sikuinayo fwata, kwa kigezo hichi akatumia kaondoka nchini na kuelekea Israel sehemu ilipo familia yake.

                                             ***

Anna akafanikiwa kununu manunuzi yote aliyo agizwa na wezake, akaelekea sehemu ya kununulia magari ambapo akaanza kutazama ni gari gani ambalo anaweza kununua,kwa bahati nzuri akabahatika kupata gari aina ya corora ambayo imetuka kidogo kwa kiasi cha pesa alicho nacho.

Akamaliza makabidhiano na wauzaji kisha akaondoka na kutafuta baa iliyopo karibu na sehemu ya kuuzia magari, hii ni kuepukana na kukamatwa na askari wa barabarni kwani gari lake bado halijamaliziwa kukamilisha baadhi ya usajili
Akaagiza soda na kunywa kunywa akivuta muda ifike saa mbili usiku aanze safari kurudi sehemu anapoishi, Simu ya ana ikaita na kuona ni namba ya Halima

“Wewe, mbona hurudi?”
“Nipo sehemu nimekaa nasubiri muda uende ende kidogo,kwani barabarani kumechafuka sana”
“Sasa ungesema sio kukaa kimya kutuweka sisi matumbo juu bwana”

“Musijali”
“Hili gari umesha lipata?”
“Ndio”
“Ni zuri au ni kimeo?”
“Zuri kiasi chake”
“Wewe sema zuri kiasi chake, utujie na kimeo hapa utakiendesha wewe mwenyewe”
“Haaa wasi wasi wenu wa nini sasa”
“Powa, jipya?”
“Jipya hakuna ni ishu ya jana ndio top story hapa mjini”
“Ahaaa powa mwaya”
“Ok”

Anna akakata simu na kuendelea kupata kinywaji,hadi in atimu mida ya saa tatu kasoro usiku akalipa pesa ya vinywaji alivyo kunywa na kuingia ndani ya gari,akapitia kwenye moja ya sheli na kujaza mafuta yatakayo mtosha kwa safari.Mwendo wa masaa mawili ukamtosha kufika kwenye handaki lao

“Nice job baby”(Kazi nzuri mtoto)
Rahab alizungumza huku akimpiga piga Anna mgongoni, usiku mzima wakawa na kazi ya kupanga mipango jinsi ya kwenda kuvamia benki ya taifa na muda maalumu walio upanga ni saa sita mchana siku inayo fwata

Kila mmoja akaamka asubuhi akiwa na shauku ya kufanya tukio la kwenda kupora pesa,Fetty akajitolea kuuvaa mwili wa jimama ambalo likambadilisha na kumfanya aonekane ni  mama mtu mzima mwenye familia kubwa.Kila mmoja akajiandaa na kuchukua silaha zake ambazo zitamsaida katika tukio zima,Kabla hawajatoka simu yao ya mezani ikaita 

“Pokea”
Anna akamuomba Rahab kuipokea simu hiyo
“Haloo”
“Dokta Will hapa nazungumza”
“Dokta vipi, mbona umetupiga na simu ya mezani?”
“Hilo halina tatizo sana, kikubwa nataka kuwaambi kuweni makini kwani kuna wanajeshi wametumwa kuja kuukagua huo msitu munapo ishi”
“Lini?”
“Unauliza lini? Wanakuja sasa hivi na wapo njia na hii taarifa nimepewa na kiongozi wao”

 ITAENDELEA....
Read More
      edit
Published September 20, 2016 by with 0 comment

RIWAYA: She is My Wife- Sehemu ya 7 & 8


Muandishi : Eddazaria g.Msulwa

Ilipoishia
Askari mmoja mwenye mwili mkubwa akamnyanyua Fetty na kumuweka begani mwake na safari ikaendelea.Fetty akayafumbua macho yake na kuona askari aliye mbebe ndio wa mwisho katika mstari wanao tembea,Kwa ustani wa hali ya juu Fetty akaichomeka mikono yeke katikati ya shingo ya askati,kwakutumia pigu akaanza kumnyonga askari huku akiwa amening'inia kwa nyuma.Mikoromo ya asakri ikawastua wenzake waliopo mbele kitendo cha wao kugeuka wakamkuta mwenzo ndio yupo kwenye hatua za mwisho huku macho yake akiwa ameyatoa njee

ENDELEA
Askari mmoja akataka kufyatua risasi ila mkuu wa masafara akamzuia,Fetty akaiachia shingo ya askari huku akiwa amehakikisha kwamba askari huyo yupo kwenye hali mbaya sana.Askari mmoja akampiga Fetty kwa kutumia kitako cha bunduki na kumfanya  Fetty ajikunje huku akitoa mguno mkali wa maumivu
“Kumbukeni kuwa,anahitajika akiwa hai”
Mkuu wao alizungumza
 
“Sawa mkuu,ila anahitaji kupata kibano kidogo”
Wakaendelea kumtazama mwenzo,ambaye hadi hapa alipo hali yake haipo vizuri sana.Vichwa vya askar vikaanza kupata moto kwani mwenzao ambaye alikuwa anakaribia kunyongwa ndio anaye fahamu njia ya bombo hilo japo imenyooka ila kuna sehemu mbele imegawanyika katika njia nne.Mwenzao anayejulikana kama inspector Julio hawezi kuendelea mbele na safari
 
“Mkuu kuna tatizo jengine limejitokea,Over”
“Nini tena inspector John? Over”
“Huyu binti alimkaba Inspector Julio,Over”
“Nyinyi mulikuwa wa hadi mwenzetu akabwe?”
Sauti ya mkuu wao ilizungumza huku akiwa anafoka,
“Mkuu alizimia,ndipo inspector Julio alipo amua kumbeba”
“Pumbavu zenu.Hakikisheni anatoka huyo binti,akiwa hai na Julio naye akiwa hai”
 
Fetty akatabasamu huku akiwatazama askari,kwani kwake kazi yake imeshaanza kuwa nyepesi kwani mtu ambaye anamuhofia ni huyu Inspector Julio,ambaye kwa mtazamo wake tu anaonekana ni mtu hatari sana katika swala zima la kutumia silaha.Askari mmoja akasimama mbele ya Fetty huku akiwa amempa mgongo akisaidiana na wezake katika kumpa huduma Inspector Julio,huku kazi yake ikiwa ni kuzifungua kamba za viatu vya Julio
 
Kwa umakini wa hali ya juu,Fetty akazichomoa funguo nyingi zinazo ning’inia kiunoni mwa askari huyo pasipo yeye mwenyewe kujua.Kwa bahati nzuri katika wingi wa funguo hizo zipatazo kumi na mbili,mbili ni funguo za pingu.

Macho ya Fetty yakawa na kazi ya kuwatazama askari jinsi wanavyo pata shida katika kumsaidi mwenzao ambaye hali yake inazidi kuwa mbaya.

Hakuna askari aliye kuwa na muda wa kumtazama Fetty kwani wanaamini kile kitako cha bunduki alicho pigwa kwenye tumbo,bado anaendelea kukisikilizia maumivu yake.Fetty akafanikiwa kufungua pingu za mikono pasipo askari yoyote kugundua.Akajaribisha kufungu mnyororo wa miguni ila akashindwa kwani hakuna funguo inayo ingiliana na kufuli alilo fungwa miguuni.
 
“Ja............ama..ani mmmim...i siwezi ku...pona.Ila,njia uki...oony......sha utaku...nja kulia...kwenye shimo lenye mlang....o wa....”
Inspector Julio alizungumza kwa shida na hakuweza kumalizia sentesi yake,mauti yakamchukua.

Inspector John akanyanyuka kwa hasira na kumfwata Fetty sehemu aliyo kaa.Kufumba na kufumbua akajikuta akirushwa juu kimo cha mbuzi  tena beberu na kutua chini kama mzigo.

Hii ni baada ya Fetty kuikutanisha miguu yake kwa pamoja,Kisha mikono yake aliikita chini na kujizungusha kwa kasi kubwa.Askari walio salia wakiwa wanamtizama mkuu wao.Fetty akajinyanyua kwa haraka na kumvaa askari aliye mchomolea funguo,akaichomoa bastola ya askari huyo ambaye alijitahii kumpiga ngumi  za mbavu Fetty
 
Bila ya huruma Fetty akafyatua risasi iliyo penya kwenye kichwa cha akari anayepambana naye na kumtuliza kimya.Askari watatu wa kiume wakazikoki kwa haraka bunduki zao na kuanza kuzifyatua risasi,ila kwa haraka sana kama tairi la gari liendalo kwa kasi sana,akawa na kazi ya kubiringika huku akiwafwata askari kwenye miguu yao mita chache kutoka alipo.

Akiwa anabiringika, bastola iliyopo mkononi mwake ikawa na kazi ya kufyatua risasi zilizo waangusha askari watatu chini na akabaki Inspector John na askari wa kike aliyetengenezwa kama yeye,na wakati wote tukio  la wezake kuangamizwa lilimpa kiwewe hadi akawa na kazi ya kuyaziba masikio yake akiziba asisikie milio ya risasi.Fetty akalala katikati ya miguu ya Inspector John huku mdomo bastola yake akiwa ameuweka kwenye sehemu za siri za Inspector John.Bunduki ya inspector John akawa ameilekezea kwenye kichwa cha Fetty ambaye macho yake yanatazamana na macho ya Inspector  John
“Shoot ni kushooti”
Fetty alizungumza huku akitabasama,na bastola yake akawa na kazi ya kuigusisha gusisha kwenye vitenesi vya Inspector John

 *************
Gari waliyopanda askari wapelelezi ikazidi kuongeza mwendo,huku kila mmoja akiwa na bastola yake mkononi.Kwa uelewa wao mkubwa katika kazi yao ya upelelezi wakagundua kuna gari tatu ambazo kwa Tanzania ni watu wachache sana ambao wanazimiliki kutokana na gharama zake kuwa ni kubwa sana.
“T upo tayari?”
“Ndio Y”
“l je?”
“Ndio Y”
“X je?”
“Ndio Y”
 
Askari hawa waliweza kupeana herufi za moja moja kurahisishana kuitana majina waliyo pewa kazini au na wazazi wao.

Y ndio kiongozi wao mkubwa ambaye ndio dereva wa gari hili ambalo kwa mtazamo wa bodi(umbo) lake la nje,inaonekana ni chakavu Ila injini yake na vifaa vingine ni vipya na inauwezo wa mwendo kasi 250 KM/H.

Kila mmoja akawa na kazi ya kuzitazama gari hizo zinazo wafwata kwa mwendo kama wanao kwenda nao
Rahab akiwa ametangulia gari lake mbele akawawashia wezake taa  huku akikanyaga breki za gari lake,akiwaashiria wapunguze mwendo.
 
“Baby’s munanisikia?” Rahab alizungumza kwa sauti ya kawaida
“Tunakupata”
“Wale jamaa,ninamashaka nao wamestukia dili”
“Kwa nini?” Ann aliuliza
“Kwa maana mwendo wao ni wamashaka mashaka”
“Haya sasa,Plan B yetu ni nini?” Halima aliuliza
“Kuwavamia bwana kwa pamoja” Agnes alishauri
“Tukiwavamia tutampataje Fetty?”
“Sasa ishu inakuwa vipi?” Rahab alizungumza
“Tuwafwateni tu” Anna alishauri
“Oya gari zetu,si zina map direction?”
“Ndio”
 
“Rahab wewe uliopo mbele tuambie,namba za gari la hao jamaa ni ngapi?”
“T234KSJ”
“Tuiingizeni hiyo namba kwenye hizi ramani zetu tutaweza kuiona kwa ishara hiyo gari kila inapo kwenda” Agnes alizungumza
“Sasa Ag wewe ndio mtaalamu wa hivi vitu sisi wezako wala hatujui”
“Ok,ngoja niingize”
 
Agnes akaiingiza namba ya gari na kwamsaada wa satellite aliweza kuiona gari ya wapelelezi kila inapo kwenda huku ikionekana kwa alama nyekundu.

Akawaelekeza wenzake jinsi ya kufanya na kila mmoja pembeni ya mskani wa gari lake kuna kioo kidogo kilicho unganishwa na sateliti na kazi yake ni kuweza kuonyesha ramani ya sehemu ambayo unahitaji kwenda au gari unayo taka kuifwata sehemu ilipo kikubwa ni kuweza kuzitambua namba za usajili wa gari hilo.

Wakaziendesha gari zao kwa mwendo wa kawaida na kuifanya gari ya wapelelezi kuzidi kutokomea,huku wakiwa hawana wasiwasi kuipoteza gari hiyo.

Wapelelezi wakaanza kupata matumaini baada ya gari tatu zinazo wafwata kuziacha nyuma sana.Gari ya wapelelezi ikafika Kimara Gas Station na wakashuka kwa haraka kwenye gari.Rahab na wezake wakalishuhudia gari la wapelelezi likiingia kwenye kituo cha gesi kilichopo Kimara.Wapelelezi wakaingia kwenye msitu wa miti ulipo hapo ambapo ndipo lilipo shimo ambalo wanatarajia kuwapokea Fetty na askari wengine
“Jamani tusishuke kwanza” Agnes alizungumza
“Kwa nini?”
 
“Hamuwezi kujua kama jamaa wamejificha wanatusubiria tushuke watushambulie”
“Hapo,umezungumza point”
Wakazisimamisha gari zao mbali kidogo na kilipo kituo cha gesi,wakisubiria kufanya kazi moja tu ya kuwashambulia askari hao pale watakapo mchukua Fetty

***************
Inspector Julio akaanza kutetemeka huku akimeza mafumba ya mate,kwani ni mwaka wa 25 sasa analitumikia jeshi la polisi,ila hajawahi kukutana na mwanake hatari kama Fetty.Kwa woga akajikuta akiminya kitufe cha kuziruhusu risasi kutoka,kwa bahari mbaya bunduki yake tayari imeisha risasi.
“Kwaheri”
 
Fetty alizungumza huku akiziruhusu risasi mbili kuchomoka kwenye bastola yake aina ya ‘browningu SFS’ na kuzichangua sehemu za siri za Inspector John,Fetty akasimama na kumtazama askari wa kike anaye fanana naye kuanzia mavazi hadi sura ya bandia aliyo valishwa.Fetty akataka kumuua  askari huyo ila akasitisha zoezi lake na kumnyanyua
“Nipe funguo nijifungue”
“Zip.....o kwa inspector John”
 
Fetty akamtazama kwa umakini askari,akachuchumaa kwa umakini huku bastola yake akiielekeza kwa askari huyo anaye itwa Rehema.Akaipapasa mifuko ya Inspector John na kuzitoa fungua nyingi.Akachagua funguo moja inayoweza kufungua kwenye mnyororo,kwa bahati nzuri akaipata.Akajifungua na kumuomba Afande Reheme kutangulia mbele huku akiwa ameshika tochi inayowasaidia kuona mbele.Wakafika kwenye njia nne tofauti,wakabaki wakiwa wamesimama wakiwa hawajui ni wapi waende
“Sema njia  ni ipi?”
“Sujui hata mimi”
 
Fetty akampiga kofi la shavu Afande Rehema huku akiwa amemnyooshea bastola
“Sema ni njia gani la sivyo nakumwaga ubongo?”
“Hii.....”
 
Afande Rehema alizungumza ili mradi aepukane na kifo cha kupigwa risasi.Japo amejitamkia ila njia aliyo ionyesha ndio sahihi.Wakaendelea na mwendo wao hadi wakafika sehemu yenye ngazi za chuma za kutokea nje.Fetty akamtanguliza afande Rehema japo amefungwa pingu za mikononi ila akajitahidi hivyo hivyo kuanza kupanda kwenda juu
 
*****************
Milio ya risasi waliyo isikia kupitia redio ya upepo,iliwachanganya sana wakuu wa polisi na kuwafanya waanze kubabaika na kuwapa taarifa wapelelezi kuwa kuna hali tete ambayo inaendelea chini walipo askari.

Mbaya zaidi kila wanapo jaribu kuwasiliana na wenzao hawakuweza kupata jibu la aina yoyote.Wapelelezi wakajiandaa kwa chochote kitakacho jitokeza kwenye shimo huku bastola zao wakiwa wameziandaa kwa umakini wa hali ya juu
Wakauona mfuniko wa shimo,ukifunguliwa na kichwa cha Afande Rehema kikatokeza,
“Musiniue”
 
Afande Rehema alizungumza huku akijitoa kwa kasi kwenye shimo.Fetty akajua kuna hali ya hatari ipo juu,akaishika bastola yake vizuri na kupandisha ngazi kwa hataka kabla hajajitokeza juu akakiona kichwa cha mpelelezi mmoja akichungulia,Mpelelezi akiwa anashangaa kati ya Rehema na Fetty yupi ni muhalifu kwani wanafanana,akastukia risasi ikipiga kwenye paji la uso wake na kumuangusha chini
 
Milio wa risasi ukawastua Rahab na wenzake,kwa haraka wakawasha magari yao na kuyasimamisha pembeni ya kituo cha gesi.Wakashuka kwa haraka kila mmoja banduki yake ikiwa mkononi.

Walinzi wa kitua cha gesi wakazidi kuchanganyikiwa kwani mlio huo wa risasi umesikika nyuma ya kituo na watu walio ingia kwenye  kituo chao hawaeleweki.Mlinzi mmoja akaikoki bunduki yake aina ya gobora,kitendo cha mlinzi kuishika bunduki yake,Anna alikiona vizuri,pasipo kuuliza ni nini mlinzi anataka kukifanya,akafyatua risasi iliyo muangusha mlinzi chini.Walinzi wengine wakalala chini kwa woga baada ya kumouona mwenzao akivuja damu nyingi
 
Wapelelezi wakabaki katika hali tata,huku kila mmoja akikataa kwenda kuchungulia kwenye shimo asije akakutwa na ktu kilicho mkuta X.

Wakiwa katika taharuki risasi zisizo na idadi zikatua mwilini mwao zikitokea nyuma yao na ukawa ndio mwisho wa maisha yao.Agnes akanza kupiga hatua za haraka akimfwata Afande Rehema aliye lala chini
“Fetty nyanyuka tuondole”
 
Fetty alianza kushua ngazi kurudi kwenye shimo ila baada ya kuisikia milio mingi ya bunduki.
“Fetty twende”
Agnes alizidi kumuita Afande Rehema baada ya kumuona anababaika.Kabla Fetty hajamalizi kushuka kwenye ngazi ya mwisho kuingia kwenye shimo akaisikia sauti ya Agnes.
“Agnes huyo sio Fetty ni polisi mimi nipo humu”
 
Fetty alizungumza huku akianza kupanda ngazi kwa haraka,Agnes akabaki akiwa ameshangaa,akamuona Fetty akichomoza kichwa kwenye shimo.Afande Rehema akajaribu kuiokota bastola ya askari mmoja aliye anguka chini.Risasi kama sita zikatua mgongoni mwake kutoka kwa Rahab.Fetty akamkimbilia Agnes na kumkumbatia
“Pole shosti”
“Asante”
 
Kabla hawajaondoka,mwanga mkali wa helcopar ya polisi iliotumwa kufika kwenye eneo hilo,ukaanza kuwamulika.Wakaanza kukimbia wakielekea mbele ya kituo walipo ziacha gari zao, kitendo cha Halima kujitokeza wakakutana na gari zipatazo kumi za polizi zikiwa zimetanda mbele ya kituo na askari wengi wakiwa na bunduki zao wakiwa wameelekezewa wao.
“WEKENI SILAHA ZENU CHINI”
“Shitii”
 
Wote watano wakabaki wakiwatazama askari huku helcopar ya polisi ikiwa inawamulika kwa mwanga mkali mweupe ambao umelifanya eneo walilo simama wao kuwa kama mchana na endepo watafanya kitu chochote cha kijinga,askari wenye bunduki wapatao thelasini wenye bunduki watazifyatua risasi zao pasipo kuwa na huruma


SHE IS MY WIFE(NI MKE WANGU)……8


“Nini tunafanya”
Rahab aliwauliza wenzake,huku taratibu mikono yake akiwa anainyanyua juu.Kila kitu ambacho kinaendelea katika eneo la kituo cha gesi,Dokta William anakifwatilia akiwa amelisimamisha gari lake mbali kidogo na eneo walilopo askari.

Kwa haraka alifungua nyuma ya gari lake kwenye buti na kutoa bunduki yake yenye uwezo wa kupiga risasi kwa masafa marefu inayoitwa ‘THE BOR SNIPER’ yenye uzito wa kilo sita na urefu wa milimita 1,038 sawa sawa na nchi 40.9 za urefu.

Akaiweka chini pembeni ya gari lake,kisha akalala na kufungua kifuniko cha lenzi inayoweza kuvuta karibu,Uzuri wa hii bunduki yake unaweza kuona muda wowote hata kama kuna giza ila kwa kutumia mwanga wa kijani uliopo kwenye lenzi yake unaweza kuona vizuri bila shida.

Akaifunga kiwambo cha kuzuia sauti.Alipo hakikisha kila kitu kipo sawa,akwakavuta kwa karibu Rahab na wezake na kuwaona wamenyoosha mikono yao juu .Pembeni na walipo jipanga  askari kuna tanki kubwa la gesi.Akapiga ishara ya msalaba kisha akafyatua risasi moja iliyoingia kwenye tanki la gesi.

Ndani ya sekunde mlipUko mkubwa wa gesi ukawarusha mbali askari karibia wote,mbaya mlipuko huo ukaendelezwa na magari yao yanayo tumia mafuta ya petrol na desel
Haikuwa kwa askari tu kurushwa,ila hata Rahab na wezake wakarushwa na kurudishwa nyuma walipo tokea.Halima akawa wa kwanza kunyanyuka,
“Jamani tuondokeni”
 
Alizungumza akiwahimiza weNzake,wakanyanyuka kwa haraka na kuanza kutokomea kwenye pori.Mitungi iliyo chimbiwa chini ya ardhi ikaanza kupata moto,mwisho wa siku ikaanza kulipuka mmoja baada ya mwIngine na kuzidi kusababisha vifo vya askari.Rubani anaye iendesha helcoptar ya polisi akachanganyikiwa sana,na jinsi moto unavyo waka.

Akaipeleka juu kidogo Helcoptar yake.Dokta William akaona kitendo cha rubani wa Helcoptar kuinyanyua juu.Akamvuta karibu rubani na bila ya huruma akamtandika risasi ya kifua na kumfanya aachie kila kitu alicho kishika na helcoptar ikaanza kurudi chini kwa kasi ya ajabu na kuingia kwenye moto mwingi wa gesi na kuzidi kuongeza mlipuko wa eneo la kituo
 
Dokta William akainyanyua bunduki yake kwa haraka na kuirudisha sehemu alipo itoa kwenye gari kisha akaingia ndani ya gari na kuondoka eneo alilopo,huku akilini mwake akiwa amejawa na mawazo mengi sana kwani kitendo ambacho amekifanya kwanza ni kinyume na sheria za nchi ya Tanzania pamoja na hata nchi yake ya Israel na endapo tukio hili litajulikana kama yeye ndio mtendaji mkuu atahukumiwa kifungo cha maisha jela au kunyongwa mbele ya halaiki ya watu.Kingine kinacho muumiza kichwa ni Fetty na wezake ambao aliwashuhudia wakirushwa na mlipoko wa tanki la gesi
 
Akatoa simu yake ambayo anawasiliana na Rahab na wezake.Akawapigia na kwabahati nzuri akazisikia sauti zao
“Mupo wapi?”
“Tupo kwenye haka kapori kalichopo nyuma ya kituo,tunakaribia kufika kwenye makazi ya watu”
“Sasa nyinyi,katokeeni katika barabara kuu maeneo ya Mbezi”
“Sawa”
 
Rahab na wezake wakabadilisha muelekeo na kuanza kukimbia kuelekea walipo elekezwa na Doktar Willian,ndani ya robo saa wakawa ameshafika Mbezi.Fetty kutokana amevaa nguo za polisi,ikawa ni nafasi nzuri kujitokeza barabarani kutazama ni wapi lilipo gari la Dokta William.
 
Dokta Willim akamuona Fetty  na kumtambua mara moja,akawasha gari lake kwani alikuwa amelisimamisha pembezoni mwa bararaba.Akafika sehemu walipo Fetty na wezake na wote kwa haraka wakaingia ndani ya gari ya dokta William aina ya Ford na kuondoka kwa mwendo wa kasi

***********
Tangu mwaka 1961 nchi ya Tanzania ilipo pata uhuru hapakuwahi kutokea tukio la kinyama lililo husisha mauaji ya askari zaidi ya thelathini kwa wakati mmoja tena wakiwa wanapambana na jeshi la polisi,isitoshe kuna baadhi ya wanachi waliokuwa katika kituo hicho nao pia wamefariki dunia.Tukio hili likaingizwa katika matukio ya kigaidi.Vilio vingi vilitanda kwenye nyumba za askari ambao wamefariki,hivyo hivyo kwa wananchi walio fariki hali ilikuwa ni moja ya kuomboleza vilio
 
Magazeti ya serikali na udaku yakatawaliwa na taarifa ya magaidi kulitingisha jeshi la polisi.Moja ya magazeti linalo itwa Story Za Eddy likatawaliwa na kichwa cha habari kilicho wakera viongozi wengi serikalini
 
(UZEMBE  WAUA ASKARI 30)
“Nitafutieni muandishi wa hili gazeti”
Mkuu wa polisi alizungumza kwa jazba,huku akiwatazama askari wake watatu walio simama mbele yake.Akaendelea kulipitia gazeti moja baada ya jingine kuangalia habari zilizo andikwa kwenye magazeti ya nchi hii.Akakutana na habari nyingine iliyo andikwa
(CHEZEA MAJAMBAWAZI WEWE,WAMEUNYUTI WENYEWE) Huku pembeni kukiwa na picha yake ya kikatuni ikitazama jinsi makatuni askari wakilipuliwa na moto wa gesi.Bwana Gudluck Nyangoi IGP wa polisi ikambidi kufumba macho yake na kuachana na habari ya kuyasoma magazeti ambayo yanazidi kuipandisha hasira yake.Akaitisha kikao cha wakuu wa jeshi la polisi nchi nzima na akawapa masaa manne wote wawe wamefika makao makuu ya polisi,hakujali wengine umbali wa mikoa yao ila tamko lake akaitaji lifanyiwe kazi mara moja
                                                                                           ************
Katika siku walizo amka na furaha ni hii ya leo,Agnes akaingia jikoni na kuwaandalia wezake kifungua kinywa cha nguvu na wote wakakutana katika meza ya chakula,pamoja na dokta William
“Fetty hongera” Agnes alizungumza
“Na nini?”
 
“Nimekukubali sana,wewe ni noma”
“Ahaa mbona kawaida”
“Ahaa,hivi ulisema wale askari uliwafanya nini ndani ya mtaro?”
“Wazembe wale,sema wamekufa ila wangekuwa hawajafa ningewashauri warudi tena mafunzoni”
Wakati Fetty na Agnes wanazungumza,dokta William akawa na kazi ya kupitia habari zinazo endelea kwenye mitandao ya kijami,akianzia na Facebook
 
“Jamani mambo sio mazuri kabisa”
“Kwa nini?” Halima aliuliza
“Huko nje mnatafutwa kama nini”
“Wametujua?”
“Hakuna picha hata moja inayo waonyesha sura zenu ila ni habari tuu”
“Doktar picha ya Fetty je?”
“Huyu picha yeke niliiona tuu,ila haijaandikwa vibaya”
“Imeandikwaje?” Fetty aliuliza
“Iliandikwa anatafutwa”
Wakabaki wakiwa wanacheka na kumfanya Dokta William kushangaa
 
“Mnacheka nini......!!?”
“Si hivyo unavyo sema kuwa haijaandikwa vibaya sana...ila anatafutwa,Doktar sasa hapo unadhani hayo maneno ni mazuri?” Rahab aliuliza huku akicheka
“Sawa tusikilizane,mimi nitaondoka mara moja kwenda Israel nyumbani.Hii ishu ikipita nitarudi”
“Dokta,pesa yetu?”
“Hiyo pesa yenu mimi nitawaingizia kila mmoja kwenye akaunti yake”
 
“Hapa sote unapo tuona hakuna hata mmoja ambaye ana akaunti benki,sasa hatujajua kama kunauwezekano wa sisi kuipata hiyo pesa”
 Anna alizungumza huku sura ya furaha ikiwa imepotea usoni mwake
“Nimewaelewa,kikubwa ni mawasiliano kati yangu mimi na nyinyi kwani hata nikiwa nje ya nchi nitaendelea kuwasiliana na nyinyi”
“Dokta mbona kama sijakuelewea? Ina maana pesa yetu ndio hakuna?”
 
Anna aliuliza huku akijiweka sawa kwenye kiti alicho kalia
“Pesa yenu ipo.Ila kwa kiasi cha pesa mbacho mnanidai chote kipo katika benki ya serikali ambayo kwa sasa akaunti zote zimefungwa kutokana na tukio la jana”
“Wewe kama wewe una kiasi gani kwenye hiyo benki?”
“Milioni mia sita”
“Mmmmm,wataifungua lini?”
“Hata mimi mwenyewe sijui”
“Wewe umejuaje?”
“Kuna mtu alinitumia meseji asubuhi”
“Ni nani?”
 
“Ni kiongozi wa juu,kwenye hiyo benki”
Swala la Dokta William kuto kuwa na pesa ya kumalizia kuwalipa Agnes na wenzake likaanza kumsumbua akili mmoja baada ya mwengine.Anna akanyanyuka na kuingia chumbani kwake na kurudi na bastola na kukaa kwenye kiti alicho kuwa amekikalia
 
“Dokta,tunakuamini tena sana.Ila mimi kwa hili bado hujanishawishi hata kidogo.Kwanza kumbuka sisi ni wasichana wadogo sana ambao kama tungeendelea kufanya kazi yetu ya kuiuza miili yetu tusinge tafutwa kwa mabaya kama hivi sasa.Sasa ninakupauchague vituu viwili,Uzungumze ni lini unatupa pesa yetu au uzungumze na huyu mjamaa hapa”
 
Anna alizungumza huku bastola akiiweka mezani,wenzake wote wakamtazama kisha wakamgeukia Dokta William
“Anna mimi nipeni masaa kadhaa nitawaletea pesa yenu”
“Huyu muongoo” Halima alidakia
“Siwadanganyi jamani”
 
“Mbona saa zote ulikuwa unajikenua kenua mbele yetu tuu?”
“Nilikuwa ninawapima kama mnaniamini au laa” Doktar William alizungumza kwa kujiamini
“Kuna vitu vya kudanganyana na vingine si vyakudanyanyana.Pesa ndio kila kitu bwana”
 
Fetty alizungumza huku akimtazama Dokta William kwa macho makali sana yasiyo na utani hata kidogo.Dokta William akasimama na kutoka nje ya handaki huku nyuma akiwa ameongozana na Fetty.Wakafika chini ya mti mmoja uliopo karibu sana na handaki lao,Dokta William akafukua kidogo na kutoa mfuko wa rambo ulio jaa pesa nyingi za kigeni.
“Duuu kumbe tunaishi na benki hapa ila hatujui chochote kinacho endelea”
 
“Si kutokana na nyinyi sio wachunguzi,mngejuaje”
Dokta Willia akampa mfuko Fetty na wote wakarudi ndani.Dokta William akawalipa kila mmoja kiasi chake anacho hitaji kulipwa.
 
“Jamani ninaondoka Tanzania leo.Mtajua ni nini cha ufanya na hizo pesa.Ila kwa ushauri sasa hivi ninawaomba msitembee tembee sana kwa maana mtakuwa munatafutwa kupindukia”
“Sawa”
Dokta William akandoka na moja kwa moja akafika nyumbani kwake ambapo alichukua nguo baadhi na kuelekea uwanja wa ndege

 
   **************
“Jamani dokta ndio hivyo ameondoka”
Rahab alizungumza huku akiwatazama wezake
“Itakuwaje sasa?”
“Ina bidi madili tujitafutie sisi wenyewe” Anna alizungumza
“Ngoja kaka nilisikia kuwa kuna pesa ambazo zipo benki ya Taifa?”
“Ndio”
 
“Sasa mnaonaje,tukapiga ishu ya mwisho kila mtu akaamua kwenda kivyake kutafuta maisha kwa mbele” Halima alitoa wazo lililo wanyamazisha wezake kwa muda
“Jamani mimi kuishi bila nyinyi mwenzenu wala siwezi” Rahab alizungumza
 
“Sote kuishi mbali mbali hatuwezi”
“Sasa inakuwaje,kwa maana kwa sasa tunatafutwa na vijipesa tulivyo navyo hivi hata tukisema tuondoke nchini huko tuanapokwenda tutapata shida”
 
“Ni kweli hicho ulicho kizungumza Fetty,kama mimi natamani siku na mimi niitwe mama fulani.Niwe na mume wangu tuishi maisha salama tuu” Rahab alizungumza
“Sawa ,ni lini tunapiga hiyo ishu?”
“Tuanze kuitafuta ramani ya benki ambayo tutakwenda kupiga tukio”
 
“Wewe Agnes tunakutegemea wewe ndio fundi mitambo,ingia kwenye kompyuta hizo ututafutie ramani ya benki tukapige tukio”
 
Agnes akasimama na kukaa kwenye kompyuta zilizopo sebleni kwao na kuanza kufanya utundu wake kwenye mtandao,baada ya dakika kadhaa akawa ameipata tamani ya jengo zima la benki kuu ya Tanzania
“Kazi imeanza”
 
 ***********
Ulinzi ukazidi kuimarishwa katika viwanja vya ndege vilivyopo nchini Tanzania,mipaka na bandari zote zipo chini ya uangalizi mkali wa polisi ambao kila unaye muona unatambua ana hasira na majambazi yalio waua wenzao.Hakuna mtu  hata mmoja ambaye alihitaji kutoka nje ya nchi pasipo kukaguliwa.
 
Simu ya dokta William inaita akiwa hatua chache kufika ulipo uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius K.Nyerere.Simu inatoka kwa mkuu wa polisi bwana Gudluck Nyangoi,mapigo ya moyo yanampasuka na kujikuta akiitazama simu kwa muda na anaamua kulisimamisha gari lake pembezoni mwa barabara na kuipokea simu kabla haijakata
“Habari yako dokta William”
“Salama tuu”
“Samahani dokta kwa kukusumbua,”
“Bila samahani”
“Tunakuhitaji hapa makao makao makuu”
“Saa ngapi?”
“Sasa hivi”
 
Simu ikakatwa na kuzidi kumuongezea wasiwasi Dokta William,akaitazama simu yake na kutaka kumpigia mkuu wa polisi bwana Gudluck Nyangoi ila akaacha.Akashuka kwenye gari na kutembea hatua kadhaa hadi ulipo uwanja wa ndege na kuzishuhudia gari nyingi zikiwa kwenye foleni na moja baada ya nyingine inakaguliwa.Akashusha pumzi nyingi huku asijue nini afanye,akarudi kwenye gari lake na kuingia.Nafsi moja inamuambia aende makao ya polisi huku nafsi nyingine ikimuambia asiende.
“Ngoja niende”
 
Akawasha gari lake na moja kwa moja akaelekea makao makuu ya polisi,akasimamisha gari lake kwenye maegesho na kushuka.Akatazama pande zote na kuona polisi wakiwa katika kazi ya kuimarisha ulinzi mkali.Baadhi ya polisi wakawa wanamtazama kwa macho makali.Akajikaza kiume na kuanza kupiga hatua za kawaidia na kungia  ndani ya ofisi
 
“Samahani dada nahitaji kuonana na mkuu” alizungumza na askari mmoja wa kike
“Ingia kwenye lifti pandisha hadi gorofa ya tano,utakunja kulia utaona kibao kidogo juu ya mlango kimendika UKUMBI WA MKUTANO,Utamkuta hapa”
 
“Asante”
Dokta William akaingia kwenye lifti kabla haijafunga wakaingia askari wawilii wenye vyeo vingi kwenye mashati yao.
“Hawa majambazi,tukiwakamata mama yangu nitawanywa damu yao hadharani”
 
“Kweli bwana,yaani nimeacha msiba wa mwanangu ninakuja kwenye hicho kikao.Naapa haki ya Mungu nikimkamata mmoja wao lazima nivunje sheria za nchi”
“Hivi mwanao ni miongoni mwa askari  walio kufa?”
“Ndio,tena ndio kwanza anamwaka wa pili kazini”
“Pole sana”
 
Dokta Williama aliendelea kuwasikiliza wakuu hawa wa polisi ambao vyeo vyao vinawatambulisha kama ma RPC kwenye mikoa yao.Lifti ikafunguka na wote wakatoka ndani ya lifti.Askari hao wakaendelea kwa mwendo wa kasi na kuingia kwenye ukumbi wa mikutano.Dokta William akajiweka sawa nguo zake na kuingia ndani ya ukumbi huu.Gafla macho yake yakatazamana na midomo ya bastola alizo elekezewa na wakuu wa polisi waliokaa kwenye viti vyao huku wakioneka kukasirishwa sana na uwepo wake

Itaendelea.......
Read More
      edit