Tuesday, November 21, 2017

Published November 21, 2017 by with 0 comment

Alichosema mwenyekiti wa Bavicha Patrobas Katambi Baada ya Kuitosa CHADEMA na Kuhamia CCM


Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bavicha, Patrobas Katambi ambaye amehamia CCM amesema kama ataitwa msaliti basi atakuwa kundi la wasaliti wa nchi hii.

Akizungumza leo Jumanne mbele ya Mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli kwenye Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), Katambi  amesema, “mambo mengi yalikuwa mrama  na watu tunapenda mabadiliko ila hatutaki kubadilika.”

"Kama nitaitwa msaliti basi nitakuwa msaliti kundi la wasaliti wa nchi hii, ukombozi ulishapatikana, siyo tunachokisema majukwaani ndiyo tunachokiishi,"

"Maisha tunayoyahubiri siyo tunayoishi, ukienda jimboni kwake, vijana kama nguvu kazi ya Taifa, tunajadili ‘personalities’ badala ya ‘issues’ mawazo mbadala," amesema.

"Niwaombe nijiunge na CCM siyo kwa sababu za madaraka ila tuijenge, CCM inatoa nafasi kwa vijana, vijana kwa upinzani ni sawa na karai katika ujenzi.”

Katika kikao hicho Rais Magufuli amesema karibu wanachama 200 wameomba kujiunga na chama hicho. Amesema kwa sasa hawatatambulishwa hadi mkutano mwingine.
Read More
      edit

Saturday, November 18, 2017

Published November 18, 2017 by with 0 comment

Waliombeza Dk. Shika ( Bilionea wa Nyumba za Lugumi) kuumbuka, adai mabilioni yake kutua Tanzania Hivi Karibuni

Bilionea wa nyumba za Lugumi aliyeteka vichwa vya habari siku za hivi karibuni, Dk. Louis Shika, amekamilisha malipo ya bima kwa ajili ya kutumiwa fedha zake kutoka nchini Urusi..

Dk. Shika aliingia matatani baada ya kushinda mnada wa uuzwaji wa nyumba za Said Lugumi hali iliyosababisha kukamatwa na polisi, lakini binafsi alisisitiza kuwa fedha hizo anazo na sasa anaelekea kuthibitisha hilo kwa kufanya mchakato wa kutumiwa fedha.

Waandishi wa habari walimkuta Dk. Shika akiwa katika huduma za mtandao wa internet katika shirika la Posta Jijini Dar es Salaam, ambao walikuwa katika ziara ya Naibu Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, Mhandisi Atashasta Nditiye na kujikuta hata mwenyewe akimshangaa bilionea huyo.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza kutuma taarifa za miamala hiyo, Dk. Shika amesema ametuma kiasi cha dola 100 ambapo anatarajia muda si mrefu ataweza kutumiwa fedha zake na kwenda kulipia asilimia 25 ya fedha zinazotakiwa katika nyumba hizo.
Alipoulizwa kama fedha hizo zikichelewa na kukuta mchakato huo wa malipo umepita, amesema kwa kujiamini, atanunua nyingine kwani Dar es Salaam kuna nyumba nyingi zinazouzwa siyo lazima hizo za Lugumi.

Kiasi hicho cha fedha, amekilipa kwa kwa Benki ya Equity kwenda Benki ya Bankok nchini Thailand, mchakato utakaomwezesha kutumiwa fedha zake na kuweza kununua nyumba hizo.

Katika hatua nyingine Dk. Shika alisifia huduma za shirika hilo na kueleza kwamba ndiyo hutuma huduma za internet katika kutuma nyaraka zake mbalimbali ndani na nje ya nchi.
Read More
      edit
Published November 18, 2017 by with 0 comment

Waziri Mkuu Canada Aijibu Serikali ya Tanzania Sakata la Bombardier Kuzuiliwa Nchini Humo

Wakati katibu mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano akiwa nchini Canada kushughulikia suala la ndege ya Bombardier, waziri mkuu wa nchi hiyo, Justin Trudeau amesema hawezi kuingilia uhuru wa mahakama ambayo anaamini itatenda haki.

Hivi karibuni Rais John Magufuli alisema amemwandikia barua waziri huyo mkuu wa Canada ili kujua hatima ya ndege hiyo.

Hata hivyo naibu waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Atashasta Nditiye alisema jana kuwa hawezi kuzungumzia jambo hilo kwa sababu waziri mkuu yupo na wao hawajapata taarifa rasmi.

“Lakini kingine naomba utambue kuwa katibu mkuu bado yupo Canada, kwa hiyo mambo mengi mimi sijayapata hadi atakaporudi aje kutu-breaf kilichojiri huko,” alisema Nditiye.

Akizindua uwanja wa ndege mjini Bukoba, Novemba 6, Rais Magufuli alisema amemwandikia barua waziri mkuu wa Canada kumuomba kuachiwa kwa ndege hiyo na amemtuma mwanasheria mkuu wa Serikali, George Masaju kwenda nchini humo kushughulikia suala hilo.

Kwenye barua yake ya majibu ambayo yameripotiwa na gazeti la National Post la nchini humo, waziri mkuu wa Canada Trudeau amesema hana cha kufanya kwa kuwa shauri hilo lipo mahakamani.

“Ni bahati mbaya kwamba suala hili limechelewesha kuwasili kwa ndege hii. Serikali ya Canada haina uwezo wa kuingilia, ila tuna imani mahakama itaamua kwa weledi na haki,” amekaririwa akisema Trudeau katika gazeti hilo.

Ndege hiyo, Bombardier Q400-8 inashikiliwa kwa amri ya mahakama nchini humo kutokana na shauri lililopo kati ya Serikali na kampuni ya Stirling Civil Engineering.

Kampuni hiyo ilikuwa na mkataba wa ujenzi wa Barabara ya Wazo Hill – Bagamoyo ambao ulivunjika kabla haujakamilika, hivyo ikaamua kukimbilia kwenye Mahakama ya Usuluhishi ya Kimataifa ambako ilishinda kesi. Baada ya kushinda kampuni hiyo ilipewa kibali cha kukamata mali za Tanzania katika nchi za Ufaransa, Uholanzi, Uingereza, Ubelgiji, Uganda na Canada.

Kwa miezi mitatu sasa, mahakama nchini Canada inaendelea kuishikilia ndege hiyo iliyonunuliwa kwa Dola 32 milioni za Marekani (zaidi ya Sh70.4 bilioni) kwa niaba ya kampuni ya Stirling inayoidai Serikali Dola 28 milioni (zaidi ya Sh61.6 bilioni) ambazo ni thamani ya mkataba uliovunjwa pamoja na riba.

Ndege hiyo ni miongoni mwa zile ambazo Rais Magufuli aliahidi kununua ikiwa ni mikakati ya kulifufua Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL).

Awali, ndege hiyo litarajiwa kuwasili nchini mwezi Julai, lakini hilo halikufanyika na Agosti 18, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, mwanasheria mkuu wa Chadema, Tundu Lissu alisema ndege hiyo imekamatwa nchini Canada na inaweza kupigwa mnada kutokana na deni ambalo Serikali inadaiwa na kampuni hiyo yenye makao yake Montreal, Canada.

Agosti 19, Serikali ilifanya mkutano na wanahabari kukanusha taarifa hizo, lakini ilikiri kuwapo mgogoro na kampuni hiyo.

Aliyekuwa kaimu mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo), Zamaradi Kawawa alisema mgogoro kuhusu ndege hiyo upo na kimsingi umetengenezwa na Watanzania ambao kwa bahati mbaya wameweka masilahi ya kisiasa na ya binafsi mbele zaidi ya masilahi ya Taifa.

Alisema Serikali ilikuwa imeanza majadiliano ya kidiplomasia kwa ajili ya kulimaliza suala hilo. Kwa sasa, ATCL inamiliki ndege mbili mpya aina ya bombardier zilizoingia nchini Septemba 2016, na imeagiza ndege nyingine tatu za aina hiyo na Boeing Dreamliner moja.

Akizungumzia mafanikio ya miaka miwili ya Rais John Magufuli hivi karibuni msemaji mkuu wa Serikali, Hassan Abbasi alisema mpaka Juni mwakani ndege zote zitakuwa zimewasili nchini.
Read More
      edit

Monday, November 13, 2017

Published November 13, 2017 by with 0 comment

Kauli ya Mbowe yaikera Serikali......Waziri Amtaka Aache Kuingilia Madaraka ya Rais

Serikali imemjia juu Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe kutokana na kauli yake kuwa Rais John Magufuli amekuwa akipendelea baadhi ya kanda katika uteuzi wake.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Watu wenye Ulemavu, Jenister Mhagama jana Jumatatu jioni alisema Mbowe anapotosha na kumtaka aache kuingilia madaraka ya Rais.

Wakati akichangia Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa 2018/2019, Ijumaa iliyopita Mbowe alienda mbali na kudai anaweza kuleta uthibitisho kama Bunge litamkata kufanya hivyo.

“Mumwambie bwana mkubwa unapoamua mambo mengine tenda haki pande zote. Lakini unapokuwa haki hiyo unaipeleka mahali fulani na unakandamiza upande mmoja unawanyima haki”

Mbowe alitolea mfano wa teuzi mbalimbali alizozifanya Rais Magufuli tangu aingie madarakani mwaka 2015, akisema hazikugawanywa kwa usawa wa mikoa kama utamaduni uliokuwepo awamu zilizopita.

Hata hivyo, jana Jumatatu jioni Jenister amesema Ibara ya 36 (1) (2)(3)(4) imempa Rais madaraka ya kuanzisha na kufuta ya nafasi za mbalimbali kwa utumishi na haijasema atazingatiwa usawa wa kanda.

“Ibara hiyo haisemi kuwa Rais wakati atakapokuwa anafanya uteuzi eti aangalie ukanda. Haisemi hivyo Ibara hiyo haisemi anavyoandaa uteuzi aaangalie makabila mbalimbali,”alisema Mhagama.

“Unasimamaje ndani ya Bunge kuhoji madaraka ambayo Rais amepewa kwa mujibu wa Katiba? Alihoji Mhagama na kutoa mifano ya teuzi tatu zilizofanywa na Rais kutoka mikoa ya Kaskazini.

“Ameteuliwa Aggrey Mwandry kutoka Siha kuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora na anafanya kazi vizuri sana. Ameteuliwa Alexander Mnyeti kuwa Mkuu wa Mkoa wa Manyara,”alisema na kuongeza

“Ameteuliwa Anna Kilango kutoka Same. Nina orodha ndefu lakini uteuzi huo unafuata madaraka ya kikatiba. Niwaombe sana wabunge tusiingile madaraka ya Rais aliyopewa kwa mujibu wa Katiba.”

Alisema Rais amekuwa akifanya teuzi mbalimbali kwa utashi wa hali ya juu na anateua watu wa kubeba dhamana ya kumsaidia kuongoza kwa niaba yake pasipo upendeleo.
Read More
      edit
Published November 13, 2017 by with 0 comment

Serikali Yatoa Majibu Bungeni Kuhusu Kujenga Uwanja wa Ndege Chato


Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo amesema kuwa uwanja wa ndege wa mkoa wa Geita unaojengwa wilayani Chato utakapokamilika utatumika kusafirisha madini, watu na vifaa.
==>Msikilize hapo chini akitoa majibu bungeni
Read More
      edit
Published November 13, 2017 by with 0 comment

Lazaro Nyalandu amjibu Waziri wa Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla

Aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu amemjibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla kuhusu tuhuma ambazo amezitoa juu yake wakati akizungumza bungeni  jana Novemba 13, 2017.

Nyalandu andika katika mtandao wa kijamii wa Instagram kuwa anasikitishwa na namna Dkt. Kigwangalla anavyotumia muda mwingi kumchafua mara baada ya yeye kutangaza kujivua uanachama wa CCM na kauli anazotoa dhidi yake ni za uongo.

Nyalandu ameandika;

INASIKITISHA sana kuona WAZIRI Kigwangalla akitumia MUDA wake ndani ya BUNGE leo kunichafua, kunidhihaki, na kusema UONGO na UZUSHI dhidi yangu, ikiwa ni NJAMA za makusudi zilizopangwa kunichafua mara baada ya mimi kukihama Chama Cha Mapinduzi -CCM. Aidha, hatua hiyo imepangwa kwa lengo la kuhakikisha kuwa hakuna kiongozi yeyote wa CCM atakayethubutu ama kudiriki tena kukihama Chama Cha Mapinduzi CCM katika Serikali hii ya awali ya tano. AIDHA, Waziri Kigwangalla anatumika VIBAYA, kwa kauli za UONGO na UZUSHI aliuanza DHIDI yangu mara tu alipoteuliwa, kwa kuanza kutoa kauli za kejeli dhidi ya UTUMISHI wangu uliotukuka ndani ya Wizara ya Maliasili na Utalii na wenye REKODI thabiti.

NIANZE na UZUSHI alioutoa Waziri Kigwangalla mapema leo BUNGENI, huku moyoni mwake akiwa anajua fika kuwa ametumwa kusema UONGO dhidi ya Waziri Nyalandu kwa lengo la kuandaa MAZINGIRA ya kumkamata na kubwa zaidi, kudhalilisha azma ya WATANZANIA ambao WAKO tayari kwa mabadiliko ya UONGOZI wa nchi kupitia UPINZANI. AIDHA, propaganda za Kigwangalla ameamua zimuhusu Waziri moja tu wa Maliasili, tangu TAIFA kupata Uhuru. Waziri huyu ni Nyalandu, jambo linalothibitisha NJAMA na Progaganda za kuzimisha MOTO na nguvu ya umma kupitia UPINZANI, hasa baada ya kitendo changu Cha kukihama CCM.

1) WAZIRI Kigwangalla amekejeli kuwa Waziri Nyalandu alitumia Fedha za Serikali kusafiri USA na mwanadada Aunt Ezekiel. -HABARI hii ilikuwa ya KUZUSHA na ilichunguzwa na vyombo vya dola 2014 na kuthibitika ilitungwa na ilikuwa ya UONGO. Katika Mkutano huo wa Washington, DC, Waziri Nyalandu alialikwa na Balozi wa Tanzania, Marekani, na alipewa RUHUSA ya maandishi na Serikali kuhutubia Mkutano huo kwa siku Moja. Wasanii wote
 
Walioalikwa, akiwepo Mwanadada Aunt Ezekiel, hawakuwa na mwaliko wa Wizara ama Serikali, bali waandaji wa Kongamano. Na Serikali haikulipa gharama zozote kwao.(Mthibiti Na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali anaweza kuthibitisha)

2) Waziri Kigwangalla amedanganya BUNGE kuwa Waziri Nyalandu alitumia helikopta kugombea URAIS 2015.
-Habari hii ni ya uzushi na UONGO, na Waziri atakuwa aidha hana BUSARA ambayo angepaswa kujiridhisha na Taarifa kabla ya kuisoma Bungeni, ama waliomtuma wamemwambia ASOME TU hivyo hivyo. UKWELI ni kuwa, Waziri Nyalandu, alipokuwa CCM, aligombea katika kinyang’anyiro cha URAIS kuomba kuteuliwa ndani ya CCM, na alitumia aidha usafiri wa MAGARI au NDEGE za kawaida kwa kulipa nauli (fixed wings pale ilipobidi), hadi mchakato ulipoisha kama uilivyoisha.
 
-AIDHA, miaka yote nikiwa Mbunge wa Singida Kaskazini, nimekuwa nikifanya kampeni za kumalizia kwa njia ya helikopta. Inawezekana Waziri Kigwangalla haelewi hili, lakini naomba nimjulishe TU kuwa matumizi ya helicopta ilipobidi yalisaidia kufika baadhi ya maeneo Jimboni kwangu wakati wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu 2000, 2005, 2010, na 2015.
-AIDHA, Mwaka 2015 nilitumia Helicopter kwa SIKU TATU za kumalizia Kampeni, na nilikodi helikopta hiyo kwa Sh milioni tano kwa siku (Jumla, milioni 15)
 
-Pia ingependeza kama hamaki za Kigwangalla zingemkumbusha kuwa Waziri Nyalandu akiwa Wizarani ALIPATIA Serikali Helikopta mpya Moja, alileta ndege kwa matumizi ya kupambana na Ujangili, Alishawishi Benki ya dunia, Ujerumani na USA kuleta mamilioni ya dola za kmarekani kusaidia mapambano hayo, na kwamba alifanikiwa Sana kutokmeza ujangili nchini. RAIS KIKWETE alikiri hili wakati wa kuzindua Tangazo la Tanzania (Tanzania, the soul of Africa). 3) Kigwangalla amezusha kuwa Waziri Nyalandu alitumia vibaya madaraka yake. Amezungumzia suala la Waziri Nyalandu kutotia sahihi TOZO mpya zilizopendekezwa na TANAPA. Jambo ambalo Waziri Kigwangalla angepaswa kulijua kabla ya kutoa kauli isiyo sahihi Bungeni ni kuwa SAKATA la TOZO za Tanapa lilijadiliwa BUNGENI mbele ya Spika Mama Anne Makinda, likiwa limeletwa na Kamati ya Lembeli, na kwa kupitia Wizara, Waziri Nyalandu alilitolea ufafanuzi na likamalizika na GN ilitolewa.
 
-SAKATA la kupandishwa ghafla kwa TOZO za mahotelini zinazojulikana kama (Fixed Rates) lilianza kabla sijawa Waziri. Aidha, kulikuwa na kesi Mahakama Kuu, ambako hadi kufikia mwaka 2012, uamuzi wa Mahakama uliyotolewa. Bado Nyalandu hakuwa Waziri. Aidha, nilipoteuliwa kama Waziri, Nikatazama SAKATA hilo ambalo lilishachukua muda mrefu sana hadi kufikia 2014, mimi nilipokuwa Waziri. Sheria inasema ”Concession Fees shall be 10% of half Board”, na kulikuwa Na GN ya Serikali kuhusu TOZO hizo, takribani kuanzia mwaka 2002. Hukumu ya Jaji wa Mahakama Kuu ilielekeza kuwa TOZO zozote mpya ni sharti zipate GN mpya, na sheria ya msingi ilitaka TOZO ziwe kwa asilimia (percentage), na sio TOZO za kukisia, (fixed rate) ambazo ndio msingi mkubwa wa kupendeleana na rushwa katika kupanga nani alipe kiwango gani Cha kodi. Baada ya kuitolea maelezo Bungeni (na hansardi Zipo), Bunge na Wizara tulikubaliana namna ya kulimaliza na ndivyo ilivyofanyika na GN ilitolewa. Uamuzi wangu kama Waziri ulizingatia matakwa ya sheria na Kanuni. Waziri Kigwangalla hajasema ukweli na amezusha kuhusu suala hili kwa sababu anazozijua mwenyewe.

4) Sakata la VITALU: Inasikitisha SANA na inatia AIBU kwamba Waziri atalihadaa BUNGE kwamba Waziri Nyalandu amehusika na kuuza VITALU au kugawa VITALU, na baya Zaidi kwa NJIA ya RUSHWA. -Sheria ya Wanyamapori inatamka wazi kuwa VITALU vitagawiwa kwa wawindaji kwa kila baada ya miaka MITANO. -Mara ya mwisho VITALU vimegawiwa Januari, 2017. Nyalandu hakuwa WAZIRI. (Waziri alikuwa Mh. Prof Maghembe)
-Kabla ya hapo, VITALU viligawiwa mwaka 2013. Nyalandu hakuwa Waziri. (Waziri alikuwa Mh Maige)
Hii ni AIBU sana na natumaini kwa Waziri Kigwangalla na wanaomtuma wangetamani sana miaka ibadilike ili isomeke Waziri Nyalandu.

5) Waziri Kigwangalla amedai kuwa Waziri Nyalandu alikuwa anafanyia Kazi katika Chumba maalumu katika hoteli ya Serena. Naomba Waziri Kigwangalla, athibitishe ni Chumba namba ngapi, na wahusika wa hoteli pia wathibitishe. Kama Waziri, nilifanya Kazi katika ofisi yangu iliyopo Wizaranya Maliasili na Utalii. Kigwangalla pia akumbuke mimi nilikuwa MTEULE wa Rais ambaye alikuwa na vyombo vya kumsaidia kusimamia Mawaziri.

6) MADAI kuwa Waziri Nyalandu ALIUZA Twiga mwaka 2011/12 ni ya AIBU, UZUSHI na UONGO kuzidi shetani mwenyewe. Mwaka 2011/12 Nyalandu alikuwa NAIBU WAZIRI wa VIWANDA na BIASHARA! Uongo huu ni wa aibu na ni kazi ya Shetani Lusifa mwenyewe, na MUNGU wa mbinguni awakemee wote wanaohusika.
 
7) Mbwembwe hizi na kusingiziwa kunakofanywa kwa makusudi baada ya mimi Nyalandu kukihama CCM ni aibu kwa TAIFA na ni matumizi mabaya sana ya MADARAKA. Aidha, ifahamike kuwa Vitisho na njama dhidi yangu na familia yangu kunakofanywa na wote wanaohusika hakutazimisha azma ya watanzania kutaka mabadiliko ya kweli nchini. Imeandikwa, WAONGO wote, sehemu yao ni katika ziwa liwakalo moto kwa kiberiki. Haki huinua Taifa, na uonevu na dhuluma ni dhambi itakayowatafuna wahusika siku zote za Maisha yao. 
— —— ——
Lazaro S. Nyalandu
Read More
      edit
Published November 13, 2017 by with 0 comment

VIDEO: Waziri Mpina Akiongelea kuhusu uchomaji wa vifaranga kutoka Kenya

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amesema serikali ilichoma vifaranga 6,400 kutoka Kenya ili kuzuia magonjwa ya ndege lakini pia mmiliki hakuwa na vibali na vifaranga havikukaguliwa.
==>Msikilize hapo chini
Read More
      edit
Published November 13, 2017 by with 0 comment

Vyama vya siasa vyatakiwa kufanya kampeni kwa kuzingatia taratibu za uchaguzi

Hussein Makame-NEC
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Semistolces Kaijage amevitaka vyama vya siasa kufanya kampeni kwa kuzingatia maadili ya Uchaguzi.

Jaji Kaijage ameyasema hayo wakati akifungua mkutano wa NEC na vyama vya siasa uliofanyika jijini Dar es Salaam jana Novemba 13 kuelekea Uchaguzi mdogo wa madiwani.

Alisema iwapo ukiukwaji au uvunjaji wa Maadili hayo utatokea, Chama au Mgombea awasilishe malalamiko hayo mbele ya Kamati husika ili ishughulikiwe kisheria.

Aliwakumbusha kuwa kwa mujibu wa kifungu cha 53 cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292 Tume inayo mamlaka ya kuruhusu kuwepo kwa Kampeni za Uchaguzi katika maeneo ya Uchaguzi na siyo Mikutano ya Vyama vya Siasa.

Hivyo, kampeni hizo zifanyike kwenye Kata husika na inategemewa kuwa Mikutano ya Kampeni italenga kuwashawishi, kwa namna ya kistaarabu, wananchi wa Kata husika ili wamchague Mgombea anayefanyiwa kampeni.

”Kwa mujibu wa kipengele cha 2.1. (c) cha Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2015 tunategemea kila Chama cha Siasa kiendelee kufanya Kampeni kwa mujibu wa ratiba. Kampeni zote zinatakiwa kuanza saa 2:00 asubuhi hadi saa 12:00 jioni,” alisema Jaji Kaijage.

Aliongeza kuwa kwa kuzingatia Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2015, Tume imekwisha kutoa ushauri kwa Viongozi wa Mikoa na Wilaya ili katika kipindi hiki cha Uchaguzi wahakikishe wanazingatia wajibu wao na ukomo wa madaraka yao katika shughuli za Uchaguzi kuanzia kipindi cha Kampeni hadi kutangazwa kwa Matokeo.

Naye Mkurugenzi wa Uchaguzi kailima Ramadhani aliaviomba Vyama vya Siasa kuwahimiza wanachama na wapenzi wao walioandikishwa kuwa Wapiga Kura wajitokeze Siku ya Uchaguzi kwenda Kupiga Kura zao bila hofu yoyote kuhusu usalama wao.

“Ni imani ya Tume kuwa Viongozi wa Vyama vya Siasa mtakuwa chachu ya kuwaongoza na kuwaelekeza wanachama, wafuasi na mashabiki wenu katika kushiriki uchaguzi kwa amani na utulivu,” alisema Kailima.

Uchaguzi Mdogo wa madiwani katika kata 43 za Tanzania Bara, unatarajiwa kufanyika tarehe 26 Novemba, 2017 ambapo wapiga kura 333,309 wanategemewa kupiga kura siku ya uchaguzi huo.
Read More
      edit
Published November 13, 2017 by with 0 comment

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Novemba 14

Read More
      edit
Published November 13, 2017 by with 0 comment

Serikali Yamuonya Zitto Kabwe.....Yatishia Kuifuta Manispaa ya Mji wa Kigoma Ujiji Inayoongozwa na Chama Chake

Serikali imeionya Manispaa ya Mji wa Kigoma Ujiji kuacha kuendelea kuwasiliana na Mpango wa Kuendesha Shughuli za Serikali kwa Uwazi (OGP) na kama ikiendelea itachukuliwa hatua kali ikiwa ni pamoja na kuvunja Baraza la Madiwani.

Hatua hiyo imekuja baada ya Serikali kujiondoa katika mpango huo mapema mwaka huu.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi Umma na Utawala Bora, George Mkuchika amesema bungeni leo Jumatatu wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT Wazalendo), Zitto Kabwe ambaye chama chake kinaongoza manispaa hiyo.

Zitto katika swali lake la nyongeza amesema kuwa nchi za Hungary na Urusi ambazo Serikali inasema nazo  zimejitoa katika mpango wa OGP ni miongoni mwa nchi zinazoendeshwa kidikteta kwa kutofuata utawala bora.

"Nchi za Hungary na Urusi zinaendeshwa bila kufuata demokrasia zinaendeshwa kidikteta ni aibu sana kwa Serikali kusema inaiga nchi ambazo zinaenda kinyume na demokrasia," amesema.

Amesema majukwaa hayo ya kimataifa yanatengeneza mahusiano na kwamba Canada ni mwenyekiti wa mpango huo.

Hata hivyo, amesema juzi ameona Rais John Magufuli amemwandikia Waziri Mkuu wa Canada kuhusu suala la Bombardier.

"Serikali haioni kwamba ingeendelea kuwa mwanachama wa OGP na mwenyekiti ni Canada hili ombi lingeshughulikiwa kwa uzito zaidi," amehoji Zitto.

Zitto amesema Manispaa ya Kigoma Ujiji ni miongoni mwa miji 15 duniani ambayo ipo katika mpango huo na kwamba Serikali inatoa kauli gani juu ya ushiriki wa mji huo  katika OGP ambayo imekuwa ikifaidika na mpango huo na miji mingine inayotaka kuingia katika mpango huo.

Akijibu hayo Mkuchika amesema Tanzania imejitia katika mpango kwa hiari yake  yenyewe na kwamba hawajaiga nchi yoyote.

"Sisi ni Taifa huru linalojitawala linalofanya matumizi yake yenyewe, bila kushurutishwa na Taifa lolote liwe dogo ama kubwa duniani," amesema.

Amesema Canada na Tanzania ni wanachama wa Jumuiya ya Madola na pia Tanzania ina ubalozi wake na hivyo kuwa mwanachama wa OGP na kutokuwa mawasiliano na nchi hiyo haiwezi kuwa tatizo.

Amesema andiko la mpango huo linasema nchi ikijiondoa uanachama na washirika wake wote shughuli na uanachama unakoma.

Hata hivyo, amesema kuwa Serikali ina taarifa kuwa Manispaa ya Kigoma Ujiji bado inaendelea na mpango huo na OGP walimwandikia waziri wa mambo ya nje kuwa bado wana nia ya kuendelea na halmashauri hiyo.

"Sasa nataka kupitia Bunge lako tukufu kuionya Manispaa ya Ujiji kutoendelea. Nchi inayozingatia utawala bora haiwezi Serikali kuu ikafanya maamuzi lakini baraza la madiwani likasema haliwezi kutekeleza. 
"Nataka nionye Halmashauri ya Kigoma Ujiji iache mara moja. Yale ni maamuzi ya Serikali na wakiendelea kufanya mawasiliano kama wanavyofanya sasa Serikali itachukua  hatua kali za kisheria na nyinyi mnajua kwenye baraza la madiwani hatua kali za kisheria ni kulivunja baraza na kuunda Tume ya Manispaa," amesema.

Mkuchika ameomba madiwani na Zitto kutoifikisha Serikali huko.

Katika swali lake la msingi Zitto amehoji kwanini Serikali imeamua kujiondoa kwenye mpango huo.

Akijibu Mkuchika amesema Serikali imejiunga na mipango ya kikanda na kimataifa mbalimbali hivyo ni maoni yake kuwa shughuli zinazotekelezwa kupitia mipango hiyo mingine kupitia vyombo mbalimbali inatosha kwa nchi kujijengea misingi imara ya uendeshaji wa shughuli za Serikali kwa uwazi kuongeza uwajibikaji na mapambano dhidi ya rushwa.

Mkuchika amesema kujitoa katika mpango huo hakuna madhara yoyote.
Read More
      edit
Published November 13, 2017 by with 0 comment

Maneno ya Diamond kwa Lulu Michael Baada ya Kuhumiwa Miaka Miwili

Mwanamuziki Diamond Platnumz amesema hukumu ya miaka miwili aliyopewa mwigizaji Elizabeth  Michael maarufu Lulu siyo adhabu bali ni mtihani ambao unalenga kumfanya kuwa imara zaidi.


Amesema mwigizaji huyo ambaye leo Jumatatu Mahakama Kuu imemhukumu kifungo cha miaka miwili jela, amechaguliwa na Mungu kwa kuwa anaamini anao uwezo wa kuhimili mikikimikiki.

Katika mtandao wa Instagram, Diamond anayetamba na wimbo Halleluyah, ameandika:  "Mwenyezi Mungu ameamua kukupa mtihani huu wewe kwa sababu anaamini wewe ni shujaa na imara...pia anaamini wewe ndio msichana pekee unayeweza kuuhimili mtihani huu... hivyo usisononeke, Make him Proud.”

Mbali na Diamond, wasanii wengine wametuma salamu za pole kwa Lulu akiwamo Wema Sepetu, Mboni Masimba, Snura, Dj Choka, Dk Cheni na wengine wengi.

Dk Cheni ambaye amekuwa karibu na Lulu kwa muda mrefu amesema huu ni wakati wa kumuombea Lulu kwa kuwa hakuna anayejua kesho atapata mkasa gani.

Katika mtandao wa Instagram aliweka picha ya Lulu na kuandika: "Tumuombee mtoto huyu kwa kuwa hakuna anayeijua kesho yake,".
Read More
      edit
Published November 13, 2017 by with 0 comment

Lulu Michael Ahukumiwa Kifungo cha Miaka Miwili Jela

Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imemhukumu kwenda jela miaka miwili muigizaji wa filamu bongo Elizabeth Michael (Lulu) ambaye alikuwa anakabiliwa na kesi ya kuua bila kukusudia.

Hukumu hiyo imetolewa leo na Jaji Sam Rumanyika aliyekuwa anaendesha kesi hiyo, na kusema kwamba mshtakiwa amekutwa na hatia ya kuua bila kukusudia kutokana na ushahidi wa mazingira, hivyo atatumikia kifungo cha miaka miwili jela.

"Ushahidi wa mazingira unaweza kutumika kama msingi pekee wa kumtia hatiani mshtakiwa tena mshtakiwa pekee, sasa ninapokwenda kuangalia maelezo ya mshtakiwa kama yanakidhi vigezo nilivyosema awali, kwa mujibu wa mshtakiwa alisema alianza kupigwa na marehemu, marehemu alilewa lakini kuhusu mshtakiwa anatakiwa kutoa maelezo yanayo jitosheleza, kwa hili mshtakiwa alijikanganya" amesema Jaji Rumanyika.

Jaji Rumanyika ameendelea kwa kusema kwamba.."mshtakiwa katika maelezo yake hakueleza kuwa marehemu alianguka au laah wakati anamkimbiza, maelezo ya Dkt. Josephine siyo maelezo ya cheti cha hospitali, hayakuwa na hadhi ya hospitali".

"Inakinzana na hekima ya kawaida kwamba hata pale marehemu alipoendelea kumpiga na kumshambulia na akaenda kiwango cha kumtishia kumuua, mstakiwa hakuthubutu hata kumpiga, ina maana alifanya kama maneno ya biblia yanavyosema mtu akikupiga shavu la kushoto mgeuzie na la kulia lakini hili mshtakiwa hakulisema.", amesema Jaji Rumanyika.

"Na wakati huo mshtakiwa alikuwa na miaka 17, leo ana miaka 22, alikuwa mtoto hivyo asingetambua kuwa kinachofanyika ni kibaya au kizuri, huyu mtoto sio mshtakiwa aliyelengwa nasheria ya watoto, kama mtoto wa umri huu na anaweza kafanya ya watu wazima,  mahakama hii haikubaliani bali mshtakiwa ni mkomavu, hakuna mashaka kuwa kifo cha marehemu kilitokana na ugomvi", ameendelea kusema Jaji Rumanyika mahakamani hapo.

Baada ya hapo jaji rumanyika aliwapa nafasi upande wa mshtakiwa kujitetea ambapo wakili wake Peter Kibatala alimtetea mshakiwa kwa kusema kuwa mshtakiwa anategemewa na familia yake.

Baada ya hapo Jaji Rumanyika alitoa hukumu yake na kumuamuru mshtakiwa kwenda jela kwa miaka miwili.

Elizabeth Michael (Lulu) anahukumiwa kwa kumuaa aliyekuwa mpenzi wake Steven Charles Kanumba ambaye pia ni muigizaji mwenzake, mnamo April 7, 2012.
Read More
      edit
Published November 13, 2017 by with 0 comment

Alichokisema Mama Kanumba Baada Ya Lulu Michael Kuhukumiwa Miaka Miwili

Mama wa Muigizaji Marehemu Steven Kanumba, Flora Mtegoa amefunguka na kusema kwamba leo atakwenda makaburi ya kinondonni alipozikwa mwanaye ili kwenda kumzika upya.

Mama Kanumba ametoa kauli hiyo muda mfupi baada ya Mahakama Kuu kumhukumu kifungo cha miaka miwili Muigizaji Elizabeth Michael ambaye alikuwa mtuhumiwa katika kesi ya mauaji bila kukusudia yaliyopelekea kifo cha muigizaji huyo.
“Namshukuru Mwenyenzi Mungu, naishukuru Mahakama imetenda haki, naishukuru Serikali yangu awamu ya tano“

“Kalale salama mwanangu Steven Kanumba na nikitoka hapa nakwenda makaburini naamini nakwenda kumzika akapumzike kwa amani”
  Mama Kanumba

Kwa upande wa Wakili wa Muigizaji Lulu Peter Kibatala ameweka wazi kwamba watakata rufaa kufuatia hukumu ya Mahakama iliyotolewa leo kwa mteja wake.

Muigizaji Lulu leo amehukumiwa kifungo cha miaka miwili jela baada ya kukutwa na hatia ya kumuua muigizaji mwenzake ambaye pia alikuwa mpenzi wake Steven Kanumba usiku wa Aprili 7 2012.
Read More
      edit
Published November 13, 2017 by with 0 comment

Mbowe Amvaa Profesa Lipumba

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Freeman Mbowe amedai kwamba Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF anayetambuliwa na msajili wa vyama Prof. Ibrahim Lipumba kuwa ni Profesa wa ajabu ambaye anaweza kubomoa chama alichokijenga.

Akiwa kwenye kampeni za uchaguzi mdogo Mtwara, Mh. Mbowe amesema kwamba hana ugomvi wowote na Prof Lipumba ingawa amekiri atakuwa muongo akisema kwamba anamuheshimu kwani anatumika katika kukivuruga chama alichokuwa akikiongoza kwa muda mrefu.

Mh. Mbowe amesema kwamba wakati CUF ikishirikiana na UKAWA kwa ujumla kutafuta kura na kuongeza wabunge wa chama hicho bungeni, yeye Prof Lipumba alikuwa mafichoni na anamshanga sasa hivi anavyorudi ndani ya chama hicho na kutaka kukisambaratisha.

"Sina ugomvi na Prof Lipumba lakini nikisema namuheshimu nitakuwa muongo sana. Prof Lipumba ni msomi sana tena msimchezee kwenye elimu lakini usomi ni jinsi unavyotumia elimu yako lakini siyo wingi wa vyeti. Ni Profesa wa ajabu kweli kweli. Mimi simuogopi mtu nitazungumza straight. Amesema Mbowe

Pamoja na hayo Mbowe amedai kwamba Spika wa Bunge pamoja na Msajili wa vyama vya siasa wanatumika katika kuibomoa CUF na kuongeza kwamba hataacha kusema ukweli kwani hakuna mtu yoyote anayemuogopa isipokuwa Mungu pekee.

Ameongeza kwamba kasi inayotumika kuibomoa CUF inatumika pia kuibomoa CHADEMA na kuweka wazi kwamaba siku chama cha Chadema kikiuliwa labda awe amefariki lakini siyo wakati huu ambao bado anapumzi.
Read More
      edit

Sunday, November 12, 2017

Published November 12, 2017 by with 0 comment

Maajabu: Tajiri Aliyeshinda Mnada Nyumba za Lugumi kwa Blioni 3.3 Anaishi Nyumba ya Kupanga....Kodi Kwa Mwezi ni 50,000

Wakati maswali mengi yakijitokeza kuhusiana na Dk. Louis Shika, ambaye aliibuka mshindi katika mnada wa nyumba za kifahari za Said Lugumi zilizoko Mbweni JKT na Upanga jijini Dar es Salaam kwa thamani ya jumla ya Sh. bilioni 3.3, imebainika kuwa anaishi katika chumba kimoja cha kupanga.

Imebainika  kuwa  Dk. Shika anakaa kwenye nyumba hiyo iliyopo Mtaa wa Amani kwa kipindi cha takribani mwaka mmoja sasa na kodi anayolipa kwa mwezi ni takribani Sh. 50,000.

Aidha, baadhi ya majirani zake wamemuelezea kuwa ni mtu asiye na makeke, huku baadhi wakidai kuwa aliwahi kuwaahidi wauza mihogo ya kukaanga walio jirani na mahala anapoishi kuwa atawaunganishia kupata mikopo nafuu ili wakuze biashara zao, lakini bila ya kuwatajia taasisi atakayowaunganisha nao. Inadaiwa kuwa vilevile, kwa baadhi ya watu hufahamika kwa jina la ‘profesa’.

Dk. Shika alijipatia umaarufu katikati ya wiki baada ya kuibuka mshindi katika mnada wa nyumba za kifahari za Lugumi, kwa kununua nyumba moja ya Mbweni kwa Sh. bilioni 1.2, nyumba ya pili iliyoko pia Mbweni Sh. milioni 900 na nyumba ya tatu iliyoko Upanga alishinda na kutaka kununua kwa Sh. bilioni 1.2.

Hata hivyo, alishindwa kutumiza masharti ya kulipa asilimia 25 ya fedha kwa kila nyumba baada ya kushinda, hivyo kujikuta akitiwa mikononi mwa vyombo vya dola kwa kuharibu mnada.

Katikati ya wiki hii, jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, lilimtia nguvuni Dk. Shika kutokana na tuhuma za kuharibu mnada huku likidai kuwa linafanya uchunguzi zaidi ili kubaini kwa nini alifanya hivyo.

Mbali na kuchunguza juu ya hatua ya kuharibu mnada, kamanda wa kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, alisema walikwenda nyumbani kwake kufanya upekuzi sambamba na kuchunguza udaktari wake. Shika aliwahi kukaririwa kuwa ni msomi wa shahada ya uzamivu (Ph.D).

Hata hivyo, Mambosasa alisema udaktari wake huo unatia shaka kwa kuwa ameshindwa kuonyesha vielelezo kuthibitisha kama anastahili hadhi hiyo.
Read More
      edit
Published November 12, 2017 by with 0 comment

HESLB yatangaza wanafunzi wengine 1,775 wa mwaka wa kwanza waliopata mikopo, Yafungua dirisha la rufaa hadi Novemba 19

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetangaza orodha nyingine yenye wanafunzi 1,775 wa Mwaka wa Kwanza waliofanikiwa kupata mikopo na hivyo kufanya jumla ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza waliopangiwa mikopo hadi sasa kufikia 31,353.
 
Katika Awamu ya Kwanza, wanafunzi 10,196 wa mwaka wa kwanza walipangiwa mikopo, Awamu ya Pili (11,481), Awamu ya Tatu (7,901). 
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana (Jumapili, Novemba 12, 2017) na Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Bw. Abdul-Razaq Badru, orodha kamili ya wanafunzi hao inapatikana katika tovuti ya Bodi (www.heslb.go.tz) na pia imetumwa kwa vyuo husika jana ili kuwawezesha wanafunzi kufanya usajili na kuendelea na masomo.

“Tumekua tukifanyia kazi orodha za udahili ambazo tumekuwa tukipokea, na kila tunapokamilisha, tunatoa orodha za wanafunzi waliopangiwa mikopo ambao wana sifa – leo tumetoa hao 1,775,” alisema Bw. Badru.

Bw. Badru, katika taarifa yake kwa vyombo vya habari pia alikumbusha kuwa kiasi cha shilingi 427.54 bilioni zimetengwa kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi kwa mwaka 2017/2018 na tayari Serikali imeshatoa shilingi 147.06 bilioni kwa ajili ya robo ya kwanza ya mwaka huu wa 2017/2018. 
Fedha hizo, shilingi 427.54, ni kwa ajili ya jumla ya wanafunzi 122,623 wa mwaka wa kwanza na wale wanaoendelea na masomo.

Wakati huohuo, HESLB imetangaza kufungua dirisha la rufaa kuanzia kesho, Jumatatu, Novemba 13, 2017 hadi Novemba 19, 2017 ili kuwapa fursa waombaji wote ambao hawajaridhika na upangaji wa mikopo kuwasilisha rufaa kupitia vyuo walivyopata udahili.  
Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji huyo wa HESLB, lengo la HESLB ni kuhakikisha wanatangaza orodha ya majina ya waombaji mikopo waliofanikiwa katika rufaa zao ifikapo au kabla ya tarehe 30 Novemba mwaka huu.

“Tunatoa wito kwa uongozi wa vyuo vyote kupokea maombi ya rufaa za wanafuzi na kuwasilisha kwa Bodi ya Mikopo kabla ya Novemba 22, 2017 ili kuiwezesha Bodi kutoa orodha ya waombaji waliofanikiwa katika rufaa zao ifikapo Novemba 30, 2017,” alisema Bw. Badru katika taarifa yake.
Maelezo ya kina kuhusu utaratibu wa kuwasilisha rufaa yatatolewa kupitia tovuti ya Bodi (www.heslb.go.tz).
Read More
      edit
Published November 12, 2017 by with 0 comment

Hatma ya Lulu kubaki uraiani au Gerezani Kujulikana Leo

Wadau wa sanaa ya filamu nchini masikio yao leo yatakuwa katika Mahakama Kuu ambako kutakuwa na tukio kubwa katika tasnia hiyo wakati itakapotolewa hukumu ya kesi inayomkabili mwigizaji maarufu nchini, Elizabeth Michael maarufu kama Lulu.

Lulu anakabiliwa na kesi ya kumuua mpenzi wake Steven Kanumba bila kukusudia, kinyume cha kifungu cha 195 cha kanuni za adhabu (PC), Aprili 7, 2012, Sinza Vatican jijini Dar es Salaam kufuatia ugomvi wa kimapenzi ulioibuka baina yao.

Hapana shaka kuwa hii ni hukumu ambayo inasubiriwa kwa hamu na wadau wa sheria, sanaa ya uigizaji, wapenzi wa filamu, ndugu, jamaa na marafiki wa mshtakiwa huyo na wa marehemu Kanumba na hata jamii kwa jumla.

Hii inatokana na ukweli kwamba ni moja ya kesi zilizovuta hisia za makundi yote katika jamii tangu kutokea kwa tukio hilo, kushtakiwa kwa msanii huyo, jinsi jamii ilivyokuwa ikifuatilia mwenendo wa kesi pamoja na kuibua mjadala mkubwa kwenye mitandao ya jamii na hata vijiweni.

Wakati upande wa mashtaka ukidai kuwa Lulu alimuua Kanumba bila kukusudia, Lulu mwenyewe mara zote amekuwa akikana mashtaka hayo akidai kuwa hahusiki kwa vyovyote na kifo cha mpenzi wake huyo.

Hata hivyo, mvutano huo baina ya mshtakiwa huyo na upande wa mashtaka unatarajiwa kuhitimishwa leo na Jaji Sam Rumanyika aliyekuwa anasikiliza kesi hiyo.

Kama ilivyo ada kwa kesi yoyote, kila upande yaani upande wa mashtaka na wa utetezi (mshtakiwa) utakuwa unatarajiwa moja kati ya mambo mawili; mshakiwa kutiwa hatiani na kuhukumiwa adhabu au kuachiwa huru.

Hivyo ndivyo inavyotarajiwa kutokea pia kwa hukumu ya msanii huyo itakaposomwa na Jaji Rumanyika na kama mshtakiwa atatiwa hatiani na kuhukumiwa kifungo au atabaki uraiani kuendelea na maisha kama kawaida, iwapo mahakama haitamtia hatiani.

Kwa vyovyote itakavyokuwa matokeo ya hukumu hiyo yatakuwa na uzito wa pekee kwa msanii huyo kwani ndiyo itakayotoa mustakabali wa maisha yake.

Hii ina maana kwamba iwapo apatikana na hatia, basi atakabiliwa na adhabu, jambo ambalo litabadili historia na mustakabali wa maisha yake kwa jumla, ingawa inategemeana na adhabu atakayopewa.

Lakini iwapo atashinda kesi hiyo, basi yeye ndiye atakayekuwa na furaha kubwa kwa kuwa atakuwa ameepuka adhabu, na hivyo kuendelea na maisha akiwa huru.

Kwa hiyo, wakati wa hukumu hiyo Jaji Rumanyika anatarajiwa ama kumtia hatiani na kumhukumu adhabu au kumwachia huru.

Katika kufanya hivyo, jaji huyo atazingatia ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na mashahidi wa pande zote, yaani upande wa mashtaka na upande wa utetezi pamoja na vielelezo mbalimbali.

Mbali na ushahidi huo na vielelezo vyake, pia Jaji Rumanyika atazingatia sheria zinazoongoza kesi za namna hiyo pamoja na uamuzi wa kesi mbalimbali zilizowahi kuamuliwa zenye mashtaka na hata mazingira yanayofafana nayo.

Katika kesi hasa za mauaji ama ya kukusudia au ya bila kukusudia huwa kuna ushahidi wa aina mbili. Mosi ni ushahidi wa moja kwa moja, yaani ushahidi wa kushuhudia tukio.

Pili, ni ushahidi wa kimazingira. Huu ni ushahidi ambao hakuna shahidi aliyeshuhudia moja kwa moja tukio likitokea, bali mshtakiwa huhusishwa na tukio kulingana na mazingira yaliyokuwapo kabla au wakati wa tukio husika.

Katika kesi ya Lulu, kwa mujibu wa Jaji Rumanyika, upande wa mashtaka umeegemea kwenye aina hii ya pili ya ushahidi wa mazingira, kwani kati ya mashahidi wanne wa upande huo hakuna hata mmoja aliyeshuhudia tukio hilo.

Ushahidi wa upande wa mashtaka unasema Kanumba alifariki dunia kutokana na tatizo la mtikisiko wa ubongo lijulikanalo kwa kitaalamu kama brain concussion, lililosababisha mfumo wa upumuaji kushindwa kufanya kazi baada ya kujibamiza ukutani upande wa kisogoni.

Hivyo upande wa mashtaka unadai kuwa mshtakiwa ndiye aliyesababisha Kanumba kujibamiza ukutani (ukimaanisha kuwa alimsukuma) na hivyo kupata tatizo lililosababisha kifo chake.

Hata hivyo, hakuna shahidi hata mmoja aliyeieleza mahakama kuwa alishudia mshtakiwa akifanya jambo ambalo lilisababisha kifo cha Kanumba, badala yake kuna ushahidi wa kusikia sauti za ugomvi baina ya Lulu na Kanumba chumbani mwa Kanumba.
Read More
      edit